Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchuzi na Mawasiliano (Ujenzi), Eng. Joseph Nyamhanga.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame M. Mbarawa(Mb), amemteua Dkt. Musa Mgwatu kuwa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA).
Dkt. Mgwatu amechukua nafasi ya Mhandisi Marcellin Magesa ambaye amepangiwa majukumu mengine Wizarani.
Kabla ya Uteuzi huo Dkt. Mgwatu alikuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika Hodhi la Rasilimali za Reli (RAHCO).
Katika hatua nyingine Profesa Mbarawa amemteua Bw. Masanja Kadogosa ambaye pia ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRL) Kukaimu nafasi ya Mtendaji Mkuu wa RAHCO.
Uteuzi huo unaanza mara moja.
Imetolewa na
Eng. Joseph M. Nyamhanga
Katibu Mkuu (Ujenzi)
Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...