Balozi Chabaka Kilumanga akipokea zawadi kutoka kwa Rais. Azzali Ousman
Kutoka Kushoto Rais Azali Ousman, Balozi wat Tanzania nchini Komoro Mhe. Chabaka Kilimunga, Bw. Mudrick Soragha Mkuu wa Afisa Ubalozi na Bi. Sheehat Kassim Mkalimani .
Mhe. Chabaka Kilumanga Balozi wa Tanzania ndani ya Muungano wa Visiwa vya Komoro leo tarehe 17 Oktoba, 2016 alikutana na kufanya mazungumzo na Mhe. Col. Azzali Ousmani, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Visiwa vya Komoro katika Ikulu ya Bait Salam. Hii ni mara ya kwanza kwa Mhe. Rais Azzali kufanya mazungumzo na Balozi huyo kutoka Tanzania tangu kuingia kwake madarakani Tarehe 25 Mei, 2016. 

Katika mazungumzo yao Mhe. Chabaka Kilumanga alichukua fursa hiyo kumpongeza Rais Azzali kwa kuchaguliwa kwa kishindo kuongoza Wanakomoro na kuelezea kuwa Tanzania itaendelea kutoa ushirikiano wake kwa Komoro hasa kwa kuzingatia mahusiano yakaribu yaliyopo baina ya hizo mbili. 

Kwa upande wake Mhe. Azzali Ousmani, Rais wa Jamhuri ya Muungao wa Visiwa vya Komoro alimshukuru Mhe. Balozi kwa ushirikiano ambao amekuwa akiupata kutoka kwa Ubalozi wa Tanzania nchini Komoro na kueleza kuwa Komoro inajifunza mambo mengi kutoka kwa ndugu zao wa Tanzania. 

Aidha aliezea kuwa uhusiano uliopo baina ya Tanzania na Komoro ni wa Kihistoria na ni matarajio yake kuwa uhasiano huo utaendelea kukuzwa na kudumishwa kwa manufaa ya nchi zote mbili. Wakati wakimaliza mazungumzo yao, Mhe. Azzali alieleza dhamira yake ya kutaka kufanya ziara nchini Tanzania na kwamba ni matarajio yake kuwa ziara hiyo itafanyika mapema iwezekanavyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...