Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa amemtaka Mkandarasi wa Kampuni ya Ujenzi ya Sinohydro Corporation anayejenga barabara ya Dodoma-Mayamaya yenye urefu wa kilometa 43.65 kukamilisha ujenzi huo ifikapo mwezi Novemba mwaka huu.

Akizungumza mara baada ya kukagua barabara hiyo mkoani Dodoma na kuridhishwa na ujenzi wake Prof. Mbarawa amesema kuwa barabara hiyo ni muhimu kwani ni kiungo kikuu kwa watu wanaosafiri kati ya mkoa wa Dodoma, Manyara, Arusha na nchi za Ukanda wa Kusini mwa Afrika.

“Kamilisheni kipande hiki kilichobaki haraka kwani barabara hii ni kiunganishi cha nchi za Kaskazini na Kusini mwa bara la Afrika hivyo kukamilika kwake kutasaidia kufungua fursa za kibiashara na kukuza uchumi wa nchi”, amesema Waziri Mbarawa. 

Amemtaka mkandarasi huyo kuzingatia viwango bora vya ujenzi wa barabara kama ilivyosainiwa kwenye mkataba na kuhakikisha thamani ya fedha katika ujenzi huo unaonekana.
Muonekano wa Barabara wa Dodoma-Mayamaya yenye urefu wa KM 43.65 ikiwa katika hatua za mwisho za ujenzi wake. Barabara hiyo inatarajiwa kukamilika mwezi Novemba Mwaka huu.
Meneja Mradi wa Barabara ya Dodoma-Mayamaya yenye urefu wa KM 43.65 Eng. Yusuf Karera, akitoa maelezo ya hatua iliyofikiwa ya ujenzi wa barabara hiyo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa (wa tatu kushoto), alipokagua ujenzi wake, Mkoani Dodoma.
Muonekano wa tabaka la kwanza la Barabara ya Dodoma-Mayamaya yenye urefu wa KM 43.65 ambayo ujenzi wake unatarajiwa kukamilika mwezi Novemba mwaka huu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...