Na Editha Karlo wa blog ya jamii,Kagera

MKOMBOZI Commercial Bank ambayo ni moja ya benki zinazokuwa kwa kasi nchini, jana imekabidhi madawati mia moja(100) kwa shule ya  Msingi Ngarama ikiwa ni katika juhudi za kuunga mkono wito wa Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli wa kuchangia madawati mashuleni.

Madawati hayo yalikabidhiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Bibi  Edwina A. Lupembe katika hafla iliyofanyika katika viwanja vya  shule hiyo na kuhudhuriwa na Mkuu wa Wilaya ya Bukoba Deodatus Kinawilo ambaye alipokea rasmi madawati hayo.

Akikabidhi madawati hayo Mkurugenzi  wa banki hiyo Edwina Lupembe  alisema wao kama benki wameguswa na tatizo hili la madawati na kuona ni jambo la busara kuchangia ili watoto waweze kusoma bila matatizo.

“Sisi Benki ya Biashara ya  Mkombozi tunathamini sana elimu na tunaunga mkono jitihada mbalimbali za serikali za kuboresha elimu hasa katika hili la madawati ambapo hapo nyuma tulishuhudia wanafunzi wengi wakikaa chini. Wahenga walisema; Kama mpango mkakati wako ni wa mwaka mmoja panda mpunga kama mpango wako ni  wa miaka kumi panda miti lakini kama mpango mkakati  wako ni wa miaka 100 somesha watoto. Wote tutakubaliana kuwa mpango mkakati wa selikali yetu katika elimu ni wa miaka 100.” alisema.

Alitumia nafasi hiyo kutoa wito kwa uongozi wa shule hiyo kuhakikisha madawati hayo yanatumiwa vizuri ili wanafunzi wengi zaidi waweze kufaidi, na kwa wanafunzi aliwataka wafanye bidii katika masomo yao kwani sasa mazingira ya kusomea yatakuwa bora zaidi na kwamba elimu ni ufunguo wa maisha bora.

Bibi  Lupembe alisema mbali na mchango katika jamii, benki yake imekuwa katika mstari wa mbele kuanzisha huduma ambazo zinalenga kuwasaidia wananchi hasa wenye kipato cha chini kama vile huduma ya mikopo ya Mfuko wa Bima ya Afya kwa wakopaji wa vikundi.

“Huduma hii ni endelevu  na napenda kutoa rai kwa wazazi na walimu waliopo hapa wajiunge katika huduma ya mikopo ya  vikundi inayotolewa na Benki ya Biashara ya Mkombozi kupitia tawi lake la hapa Bukoba ambavyo vitawasaidia kupata mikopo hii ya Mfuko wa Bima ya Afya wa Taifa,alisema na kuongeza kuwa hii italeta afueni kubwa kwani wanafunzi pia wataweza kulipiwa kadi zao za matibabu kupitia bima za wazazi wao ambao watakuwa wamejiunga na vikundi vya mikopo kutoka Benki ya Biashara ya  Mkombozi.
 Mkurugenzi wa benki ya Mkombozi, Edwina Lupembe akikabidhi msaada wa madawati 100 kwa shule ya msingi Ngarama Wilayani Karagwe kwa Mkuu wa Wilaya ya Bukoba mjini
 Viongozi wa Wilaya ya Karagwe na viongozi wa banki ya mkombozi wakiwa wamekaa kwenye moja ya dawati yaliyotolewa msaada na banki ya mkombozi kwa shule ya msingi Ngarama.
  Wanafunzi wa shule msingi Ngarama wakifurahia madawati waliyopewa msaada na banki ya mkomboz

 Wanafunzi wa shule ya msingi Ngarama wakibeba madawati yao waliyopewa msaada na banki ya mkombozi.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Madawati hayana ubunifu, staili ile ile ya miaka ya 1960. Sijaponda juhudi bali naomba juhudi za ubunifu ziwepo.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...