Na Dotto Mwaibale

WASAIDIZI wa kisheria katika masoko ya Manispaa za Ilala na Temeke na wadau  mbalimbali wameanza kupitia mwongozo wa kupambana na ukatili wa kijinsia masokoni ulioandaliwa na shirika lisilo la Serikali la Equality for Growth (EfG) utakaosaidia kuwabana watu wanaofanya vitendo hivyo katika masoko mbalimbali.

Mwongozo huo unatajwa kuwa moja ya sababu kubwa zitakazosaidia kupunguza vitendo vya ukatili katika masoko ambavyo vinaonekana kukithiri, huku waathirika wakubwa wakiwa ni wanawake.

Akizungumza wakati wa warsha ya kiufundi ya kupitia mwongozo huo Dar es Salaam leo, Ofisa Mradi wa Mpe Riziki si Matusi unaoendeshwa na shirika hilo, Suzan Sita alisema, mwongozo huo umeandaliwa kukabiliana na vitendo vya ukatili ambavyo vilikuwa havizingatiwi kwa ukaribu.

Alisema shirika hilo lilifanya utafiti ambao ulionesha kuwa japo kuna asilimia kubwa ya wanawake wanaokumbana na vitendo vya ukatili wa kijinsia hwaripoti popote huku wale wanaoripoti utatuzi wa miggoro yao hauridhishi.

“Hata wakati wa utayarishaji wa mwongozo huu, ilidhihirika kwamba kuna sekta zinazotoa huduma mbalimbali hazishirikishwi kikamilifu… Mapendekezo yaliyotolewa na wadau wengi ni kuboresha utaratibu uliopo,” alisema Sita.

Alisema shirika hilo limeshirikiana na Ofisi ya Manispaa ya Ilala, Idara ya Ustawi wa Jamii, Ofisi ya Diwani Ilala pamoja na taasisi zingine kuandaa mwongozo huo.
 Mwezeshaji wa Kisheria katika Soko la Ilala Mchikichini, Charles Beatus (kulia), akiwaongoza wenzake kupitia mwongozo wa kuzuia na kupambana na ukatili wa kijinsia masokoni jijini Dar es Salaam leo. Mwongozo huo umeandaliwa na Shiriki la Equality for Growth (EfG). Kutoka kushoto ni msaidi wa kisheria kutoka Soko la Tabata Muslim,  Saada Juma na Said Mnijuka kutoka Soko la Ilala Mchikichini.
 Mwanasheria wa Manispaa ya Ilala, Bonaventule  Mwambaja (kulia), akitoa mada kwa wawezeshaji wa kisheria masokoni na wadau wengine.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...