Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa
Barabara nchini (RFB), Bw. Joseph Haule akifafanua jambo kwa waandishi
wa habari kuhusu ripoti ya ukaguzi wa kiufundi kwa kazi ya Ujenzi wa
barabara ya Masjid Quba (KM 2.478) kwa kiwango cha lami katika Manispaa
ya Kinondoni. Jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa
Barabara nchini Bw. Joseph Haule akifafanua jambo kwa waandishi wa
habari kuhusu ripoti ya ukaguzi wa kiufundi kwa kazi ya Ujenzi wa
barabara ya Masjid Quba (KM 2.478) kwa kiwango cha lami katika Manispaa
ya Kinondoni. Jijini Dar es Salaam.Kushoto ni Kaimu Meneja wa Mfuko huo
Bw. Eliud Nyauhenga.
Baadhi ya Watendaji wa Bodi ya
Mfuko wa Barabara nchini (RFB) wakimsiliza Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko
huo Bw. Joseph Haule (hayupo pichani), wakati alipotoa ripoti ya ukaguzi
wa kiufundi kwa kazi ya Ujenzi wa barabara ya Masjid Quba (KM 2.478)
kwa kiwango cha lami katika Manispaa ya Kinondoni.Jijini Dar es Salaam
Na Chalila Kibuda,
Globu ya Jamii
Globu ya Jamii
Bodi ya Mfuko wa Barabara umesitisha ufadhili miradi ya barabara kwa Manispaa ya Kinondoni baada kubainika kutengeneza barabara chini ya kiwango pamoja na ukiukaji sheria za manunuzi.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Joseph Haule amesema kusitisha ufadhili kwa barabara kwa Manispaa ya Kinondoni kumetokana manispaa hiyo kujenga barabara chini ya kiwango ikiwemo Barabara ya Masjid-Quba iliyopo Sinza.
Haule amesema barabara barabara hiyo mkandarasi anafanya kazi huku Bodi ikiwa imetoa Sh.Bilioni 3.3 lakini Manispaa imemlipa Mkandarasi sh.milioni 200 ambapo ni kinyume na sheria ya manunuzi ya kulipwa sh.milioni 801 kwa mkupuo wa kwanza.
Amesema barabara hiyo ilitakiwa kuisha mwaka jana lakini bado wanaendelea kujenga ambapo ni kinyume cha mkataba na kuhoji kuwa mkandarasi huyo anaendelea kujenga kwa mkataba gani wakati muda wake wa ujenzi ulikuwa umeisha.
Bodi imeuagiza Katibu Mkuu wa Tamisemi kuwachukulia hatua wote waliohusika na mkataba wa barabara ya Masjid Kuba pamoja kubadili mfumo manispaa jinsi kuweza kufanya fedha ya serikali inayotengwa na Barabar inakuwa salama.
Aidha bodi hiyo imetaka Halmashauri zote kuhakikisha zinasimamia fedha za barabara ipasavyo na pamoja na barababaea kujengwa kwa ubora unaotakiwa..
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...