Bondia
Abdallah Pazi a.k.a Dullah Mbabe (78.2KG) akitangazwa mshindi mara
baada ya kumpiga kwa 'KnockOut' Bondia Chengbo Zheng (77.9KG) kutoka
nchini China katika raundi kwanza kabisa ya mpambano wao usiokuwa wa
Ubingwa uliomalizika usiku huu katika Ukumbi wa Diamond Jubilee, Jijini
Dar es salaam.
Bondia
Abdallah Pazi a.k.a Dullah Mbabe akimsukumia makonde mazito Bondia
Chengbo Zheng kutoka nchini China na kupelekea mpambano huo kuisha ndani
ya dakika mbili na sekunde kadhaa kwa 'KnockOut' ya kiufundi, katika
Ukumbi wa Diamond Jubilee, Jijini Dar es salaam.
Bondia
Abdallah Pazi a.k.a Dullah Mbabe akiendelea kumsukumia makonde mazito
Bondia Chengbo Zheng yaliyompelekea kwenda chini na kuomba kutoendelea
na mpambani huo.
Katika
mambano ya utangulizi, kulikuwa na pambano hili la raundi nane
lililokuwa na mvuto wa aina yake lililowakutanisha mabondia Said Mbelwa
(nyeupe) na Shaban Kaoneka. hili lilikuwa na pambano la rusha nirushe,
ambapo Bondia Said Mbelwa alifanikiwa kushinda kwa 'KnockOut' ya
kiufundi dakika ya saba ya mpambano huo.
Bondia Paul Kamata (nyeupe) akimsukumia makonde mithili ya mvua Bondia Buta Obed katika mpambano wao usio na ubingwa wa raundi nani, ulichezwa usiku wa leo katika Ukumbi wa Diamond Jubilee, Jijini Dar es salaam. Bondia Paul Kamata alishinda kwa 'KnockOut' ya kiufundi, katika raundi ya tano ya mchezo hio.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...