Tarehe 28/9/2016 Ilikua ni siku ya heshima kubwa sana kwa Mtanzania mzalendo Issa Kapande maarufu kama chef Issa kupata mualiko wa kujumuika katika chakula maalumu cha jioni  kilichoandaliwa Hotel National Luzern Switzerland maalumu kwa Alumni (wahitimu) 50 tu bora waliofanikiwa kitaaluma na kifani katika biashara au ajira toka pande zote za dunia kuanzia chuo kilipoanzishwa miaka 25 iliyopita.
Tarehe 29/10/2016 Ilikua ni siku maalumu ya maadhimisho ya siku ya kuzaliwa kwa chuo cha IMI miaka 25 iliyopita,  chuo hiki ni moja ya vyuo bora vya fani ya hotel na utalii nchini Switzerland. Sherehe ziliudhuliwa na watu mbali mbali toka mataifa 30 duniani.
Kwa ufupi Chef Issa ni mpishi wa kimataifa mzalendo anaeipeperusha vyema bendera ya taifa letu la Tanzania kwa kushinda tuzo mbali mbali katika mashindano mbali mbali duniani. Chef Issa ni mmiliki wa mgahawa mkubwa kuliko yote ya Kiafrika balani Ulaya ujulikanao kwa jina Tanzanian Restaurant. 
Pia chef Issa amekua akifundisha mpishi kwa njia ya blog www.activechef.blogspot.com hapo utaweza pata mafunzo ya mapishi ya kila aina. 

Kwa kupata taarifa zaidi za unaweza like Facebook page hii:
Habari nzuri kwa Watanzania ni kwamba Chef Issa ameweza kupigania na kupata nafasi za upendeleo kwa Mtanzania yeyote yule atakaependa kwenda kusoma fani ya hotel na utalii chuo cha IMI international Hotel Management Institute Switzerland atapewa nafuu ya ada na chuo kitamsimamia kupata leaving and work permit kipindi chote atakachokua masimoni. 
Kama una mwanao au ndugu yako basi wasiliana na Chef issa kwa email active.chef@yahoo.com 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...