Na Humphrey Shao,Globu ya Jamii-ILEJE

KIONGOZI wa machifu wa kindali Wilayani Ileje , Chifu Etisoni Musomba amempongeza Rais John Pombe Magufuli kwa utendaji wake tangu alipochaguliwa kuongoza taifa hili.

Chief Musomba amesema hayo katika mahojiano maalum na Globu ya jamii juu ya namna gani utawala wa jadi unavyoona mwenendo wa serikali.

“Kiukweli kwa sasa hali ni nzuri maana kumekuwa na heshima ya kutosha hata watumishi wa serikali huku vijijini tumewaona wakifanya kazi kwa bidii kutokana na kuogopa kufukuzwa tofauti na awali ambapo walikuwa wanafanya wanavyotaka na machifu tulipokemea tulidharauriwa” amesema Chief Musomba.

Chief Musomba ameongeza kuwa vijiji vimekuwa  na amani sana,watoto wanapata elimu bure na wazazi hawasumbuliwi kuhusu fedha za ada wala michango mengine iliyokuwa kero kwao.

Amesema kuwa hapo awali wazazi walilazimika kuuza mifugo yao na kuingia katika umaskini mkubwa kutokana na kulipia Ada za watoto wao pindi wanapochaguliwa kwenda Sekondari bali kwa sasa fedha kidogo wanazopata kutokana na uuzaji wa mazo zinawatosha kujikimu katika kutatu matatizo ya watoto wa shule.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...