Mkuu wa Wilaya ya longido Ndugu Daniel Godfrey Chongolo akishiriki ujenzi wa madarasa mawili katika shule ya msingi Lanchi iliyopo wilayani humo.
....................

Mkuu wa wilaya ya Longido Bw. Daniel Godfrey Chongolo ameshiriki ujenzi wa madarasa mawili katika shule ya msingi Lanchi iliyopo wilayani Longido. Shule hiyo ambayo ina wanafunzi mpaka wa darasa la tano, ilikuwa na madarasa mawili tu jambo lililosababisha shughuli za utoaji elimu kwa wanafunzi kuwa ngumu.

Katika kuhakikisha changamoto hiyo inatatuliwa, Mkuu wa Wilaya akiongozana na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Longido Bw. Jumaa Mhina wamefanya kazi ya ujenzi kwa kushirikiana na wananchi siku nzima ya leo. Katika hatua nyingine mkuu huyo wa Wilaya ya Longido aliendesha harambee iliyofanikisha kupatikana kwa jumla ya shilingi milioni 10.
Wananchi wilayani Longido wakiwa katika harakati za Ujenzi wa vyumba viwili vya Madarasa kwenye shule ya Msingi Lanchi, baada ya kuhamasishwa na mkuu wa Wilaya hiyo Ndugu Daniel Godfrey Chongolo.

Kazi ya Ujenzi wa vyumba viwili vya Madarasa katika Shule ya Msingi Lanchi wilayani Longido ikiendelea..
Mkuu wa Wilaya ya Longindo Ndugu Daniel Godfrey Chongolo akiendelea kushiriki Ujenzi wa vyumba viwili vya Madarasa katika Shule ya Msingi Lanchi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...