Na Humphrey Shao, Blog ya Jamii

Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema amekutana na wajumbe wa baraza la ardhi la wilaya hiyo na kupanga mikakati ya kutatua migogoro katika kata mbalimbali.

Akizungumza na Waandishi wa habari ofisini kwake jana Mjema alisema kuwa kuanzia sasa ataanza kuzunguka na wajumbe hao wa baraza katika kata mbalimbali ili waweze kujionea kwa macho tatizo la migogoro ya ardhi linalo wakabili.

“Hiki ni kikao cha kawaida tu chenye lengo la kupanga mipango mbalimbali ya kutatua changamoto zinazo wakabili wakazi wa Ilala haswa Migogoro ya ardhi” anasema Dc Mjema

Alisema lengo la ziara ni pamoja na kujenga mshikamano wa kikazi baina ya wananchi na Watendaji wa Serikali katika kutatua kero zao.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...