Mkuu wa Wilaya ya Ilala Sophia Mjema, akizungumza na wakazi wa kata ya Msongola katika ziara za kusikiliza na kutatua kero za wananchi katika wilaya hiyo.
 Mtendaji mkuu wa Kampunia ya upimaji na uuzaji Viwanja ya Tanzania Remex, Ali Hamadi, akiwaonyesha baadhi ya wakazi wa kata ya Msongola ramaninya mipango miji katika eneo hilo .
Katibu tawala wa Wilaya ya Ilala, Edward Mpogoro, akizungumza na wananchi wa Kata ya Msongola wakati wa ziara ya kutatua kero za wananchi katika maeneo yao . 

Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii.
MKUU wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema, amesikiliza kero 126 za wananchi wakati wa ziara yake katika kata tatu za Vingunguti, Pugu, Gongolamboto na Msongola na kuipa wiki tatu kampuni ya Tanzania Remix kuwapatia wananchi hati zao za viwanja.

Mjema amesema kuwa wananchi hao wamesubiri kwa miaka mitatu sasa juu ya mpango huo bila kuona matumaini, hivyo hakuna haja ya kuendelea kusubiri.

"Sasa natoa wiki tatu kuhakikisha fidia za wenye viwanja zinapatikana na baada ya wiki mbili kila mmoja awe amepatiwa hati yake ambayo itamuwezesha kuuza au kukopa katika mabenki mbalimbali"amesema Dc Mjema.

Dc Mjema pia alivitaka vyombo vya ulinzi na usalama kuhakikisha wanasimamia ulinzi katika kata ya Msongola kutokana na kukithiri kwa vitendo vya uporaji na mauaji.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...