DIWANI wa Kata ya Vigwaza wilayani Chalinze, Mohsin Bharwani, amemkumbuka Mwalimu Nyerere kwa kumwaga madawa katika Zahanati ya Vigwaza na Ruvu Darajani, wilayani Chalinze Mkoa wa Pwani zenye thamani zaidi ya Sh milioni 4 .

Akizungumza na wananchi wa Kata ya Vigwaza diwani huyo alisema kutokana na changamoto za ukosefu wa dawa zanazozikabili zahanati ya hizo wananchi wengi wanapata shida sana ya kukosa matibabu, hivyo yeye kama Diwani wao aliliona hilo na kuwakumbuka kwa kuwatelea dawa katika zahanati hizo ili kurahisisha matibabu kwa wananchi wake.
Diwani wa Kata ya Vigwaza wilayani Chalinze, Mohsin Bharwani akizungumza na wananchi wake waliojitokeza katika Zahanati ya Ruvu Darajani, alipotembelea na kukabidhi msaada wa dawa. 
Diwani wa Kata ya Vigwaza wilayani Chalinze, Mohsin Bharwani(CCM), akimkabidhi msaada wa dawa Mganga Mkuu wa Zahanati ya Ruvu Darajani, Dk. Gilbert Daniel, ikiwa ni sehemu ya kumuenzi na kukumbuka miaka 17 ya kifo cha Mwalimu Julius Nyerere, Oktoba 14, 2016.
Picha ya pamoja na wananchi wake hao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...