Na Humphrey Shao, 
Globu ya Jamii

Waziri wa katiba na Sheria Dkt. Harrison Mwakyembe ametajwa kuwa mgeni rasmi katika mahadhimisho ya miaka 50 ya tume hiyo katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.
Hayo yamesemwa na Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala bora, Iddi Ramadhani Mapuri, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa idara ya Habari maelezo, jijini Dar es salaam.
"Maadhimisho haya yanalenga kuangalia uzoefu tulioupata na kujifunza kutokana na mafanikio au mapungufu na changamoto zilizojitokeza katika kipindi hicho kwa lengola kuangalia hali ilivyo hivi sasa ,ikiwa ni tathmini ya kuona iwapo TKU ilifika matarajio ya wananchiau lamna kuona jinsi ambavyo THBUB imeendelea na majukumu ya TKU tangu mwaka 2001 hadi sasa"amesema Mapuri.
Ameongeza kuwa maadhimisho hayo yatatumika kutambua michango ya watu mbalimbali katika kuinua masuala ya utawala bora wa nchi.
Alitaja kuwa miongoni mwa watu wengine watakaoshiriki ni Jaji Mstaafu Gad Mjemmas, Profesa Paragamba Kabudi na Jaji Mstaafu Damiani Lubuva.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...