Na Emmanuel Masaka
Kituo bora cha redio cha EFM 93.7 kinaendelea na harakati za kuwasaidia na kuwainua vijana wanaojihusisha na muziki kupitia zoezi maalumu la "Singeli michano" linalofanyika kila siku za Jumamosi kuanzia saa nne hadi saa sita mchana.
Zoezi hili ni endelevu na litadumu kwa muda wa wiki 12 katika maeneo mbalimbali ya Dar es salaam na Pwani ambapo muziki mnene utafika.
Jumla ya wasanii 5 huibuka na ushindi na washindi hawa hupatikana kila eneo ambapo zoezi hili la kusaka vipaji vipya vya Singeli Michano hufanyika.
Meneja matukio na mawasiliano wa EFM redio Neema Mukuarsi amesema baada ya zoezi hili wasani hawa chipukizi watapata semina kutoka TCRA, BASATA na TRA ukumbi wa Dar Live Mbagala siku ya Ijumaa tarehe 14.10.2016 kuanzia saa 8:00 mchana ili kupatiwa elimu ya kulipa kodi na kuhakikisha nyimbo zao zinakuwa na maadili katika jamii.
Msaani chipukizi, Jfari Salumu a.k.a Winnero akionesha uwezo wake jukwaani katika tamasha la kusaka vipaji vya kuimba nyimbo za Singeli jijini Dar es Salaam.
Msaani chipukizi,Ramadhani Iddi a.k.a Sindano Simba akionesha uwezo wake jukwaani
Sehemu ya mashabiki wa mziki wa nyimbo za singeli wakiwa katika tamasha hilo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...