Mkuu wa Kitengo cha Fedha wa Benki ya Exim, Seleman Mponda akishirikiana na wafanyakazi wa benki hiyo tawi la Temeke kukata utepe kuashiria uzinduzi wa Tawi la Temeke jijini Dar es Salaam.

BENKI ya Exim imefanya maboresho ya huduma zinazotolewa kwa wateja wake wa maeneo ya Temeke, jijini Dar es Salaam kwa kufungua tawi jipya ambalo lina maboresho mengi tofauti na jengo ambalo walikuwa wakilitumia awali.

Akizungumza katika uzinduzi huo, Mkuu wa Kitengo cha Fedha wa Benki ya Exim, Seleman Mponda amesema kwasasa wamedhamiria kuboresha huduma zao katika maeneo mbalimbali na kuahidi wateja kuendelea kuwapatia huduma bora. 

“Benki yetu inaendelea kufanya vizuri na tumejipanga kuendelea kuboresha huduma zetu, mwanzoni tulikuwa sehemu nyingine na wateja wetu walikuwa wakituuliza lini tutahamia sehemu iliyo na nafasi nzuri ya kutoa huduma na sasa tumeipata,” alisema Mponda. 
Wageni waalikwa wakikata keki. Wa kwanza kushoto (mwenye suti nyeusi) ni Mkuu wa Kitengo cha Fedha wa Benki ya Exim, Seleman Mponda, Mteja wa Benki ya Exim, Abdelsamad Hussein, Afisa Mauzo wa Benki ya Exim Temeke, Rashid Bundara, Mteja wa Benki ya Exim, Saamu Omary, Mteja wa Benki ya Exim, Shukran Ezekiel.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...