Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Halotel Tanzania, Le Van Dai (katikati), Afisa Mtendaji wa Halotel Tanzania, Henry Mavulla (mwenye tai), Afisa Mawasiliano wa Halotel Tanzania, Stella Pius wakikata keki kwa pamoja ikiwa ni ishara ya kusherehekea kuadhimisha mwaka mmoja wa kutoka huduma ya mawasiliano hapa nchini na kuzindua huduma yao mpya ya ya HALOPESA, hafla hiyo imefanyika leo Oktoba 13, 2016 kwenye ofisi zao zilizopo eneo la Kinondoni Moroco, jijini Dar es salaam. Wengine pichani ni sehemu ya wafanyakazi wa Kampuni hiyo walioshiriki kwenye hafla hiyo.
 Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Halotel Tanzania, Le Van Dai akizungumza na waandishi wa habari wakati wa hafla yao ya kusherehekea kuadhimisha mwaka mmoja wa kutoka huduma ya mawasiliano hapa nchini na kuzindua huduma yao mpya ya ya HALOPESA, ambapo alisema kuwa lengo la Kampuni hiyo ni kuhakikisha wanawazidi washindani wao katika soko na ndio maana huduma zao zimekuwa zikipokelewa vyema sokoni.
Afisa Mawasiliano wa Halotel Tanzania, Stella Pius akizungumza na waandishi wa habari, juu ya kampuni yao inavyoendelea kuboresha miundombinu ya kijamii kama vile utoaji wa huduma ya bure ya mtandao wa intaneti kwa shule 450 hapa nchini (zenye umeme) kwa kipindi cha miaka mitatu. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...