Jaji Mkuu wa Australia ya Kusini, Mhe. Christopher Kourakis (kushoto), akipokea zawadi ya picha kutoka kwa Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Mohamed Chande Othman (kulia) katika halfla fupi iliyofanyika leo tarehe 7.10 .2016 kwenye ukumbi wa maktaba wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania.
Jaji Mkuu wa Australia ya Kusini, Mhe. Christopher Kourakis (kulia) akizungumza kuhusu ziara yake ya siku tatu aliyoifanya nchini na kubadilishana uzoefu wa masuala mbalimbali ya mafunzo, sheria na shughuli za kimahakama baina ya nchi hizo mbili. (Kushoto) ni Waziri wa Katiba na Sheria,Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe. Mkutano huo ulifanyika leo tarehe 7.10.2016 kwenye ukumbi wa mikutano wa Wizara ya Katiba na Sheria uliopo jijini Dar es Salaam.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...