Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

Sheria namba 1.
5: Goal Area
Ni mistari miwili iliyochorwa ndani ya eneo la goli ikiwa ni 5.5m sawa na 6yadi

6:Penalty area
Ni eneo la ndani ya boksi ambalo ni 16.5m sawa na 18yad ambapo ndani ya eneo hilo kuna alama ya penati inayotumika kuweka mpira.

*penalt mark
Katika eneo la penati alama ya kupigia ipo katikati ya eneo la 18 lakini lenyewe ni 11m sawa na 12yad.

*penalty arch 
Ni eneo ambalo mchezaji atakapokuwa anapiga penati asivuke nusu duara lilipo nje ya boksi na akivuka hapo penat itarudiwa.

7: The Corner Area
Linajulikana kama eneo la kona na likitambuliwa kwa alama ya nusu duara kutoka katika mti kibendera ambapo urefu ni sawa  1yad.

8:Flagposts

Ni kibendera kinachotumika katika kila kona ya uwanja na kisheria kinatakiwa kuwa futi 5 kwenda juu.
. katika Uwanja una uwezo wa kuweka vibendera 6 katila kila alama.

9:Technical Area
Ni sehemu wanayokaa benchi la ufundi na wachezaji wa akiba. Katika eneo hilo haruhusiwi mtu asiye ndani ya benchi la ufundi au kiongozi kuingia au kukaa.

*1m kutoka touchline kutakuwa na mstari utakaotambulisha mwisho wa mtu yoyote kutoka benchi la ufundi kuvuka ambao uoana wake unaendana sambamba na mistari yote ya uwanjani.

10: Goals
Goli linajumuisha milingoti miwili iliyo nyoofu kwenda juu na mmoja uliolala ikiunganisha milingoti miwili na kupata mfano wa umbo la mstatili  ambapo milingoti hiyo lazima iwe meupe na vipimo sawa  vya 12cm sawa na 5Inchi.

*Urefu wa mlingoti wa juu uliolala ni 7.32 sawa na  8yadi ambao ni kutoka mlingoti mmoha hadi mwingine.

*urefu kutoka mlingoti nyoofu kuanzia chini mpaka juj ni 2.44m sawa na 8ft.

*Kama mti wa goli ukichomoka basi mpira utasimama mpaka pale utakaporekebishwa.

Kipengele cha 11 Goal line technology (ni kipana zaidi)

12: Commercial Adv 
Matangazo yote yanatakiwa yakae 
1m kutoka  touchline , goal line na goal net hayaruhusiwi kukaa ndani ya maeneo ya Uwanja.

13: Logos And Emblems
Itaendelea sehemu ya tatu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...