Maafisa Watendaji wa SUMA – JKT katika mradi wa Uzalishaji kokoto wa SUMA – JKT uliopo Pongwe Msungula wakimtembeza katika maeneo mbalimbali Kamishna Jenerali wa Magereza, CGP- John Casmir Minja(wa tatu kulia) alipofanya ziara ya mafunzo katika mradi huo(kulia) ni Meneja Fedha na Utawala katika Mradi huo, Bi. Glory Kimaro.
Meneja Uzalishaji wa mradi wa kokoto, Kepteni Paul Mbeya akimuonesha mtambo wa uzalishaji kokoto Kamishna Jenerali wa Magereza, CGP- John Casmir Minja(kulia).
Mtambo wa Uzalishaji katika mradi wa Uzalishaji kokoto wa SUMA – JKT uliopo Pongwe Msungula kama unavyoonekana katika picha. Shirika la Uzalishaji Mali la Magereza linatarajia kuanzisha mradi wa Uzalishaji kokoto katika eneo la Gereza Msalato, Mkoani Dodoma.
Meneja Mkuu wa Mradi wa Uzalishaji kokoto wa SUMA – JKT, Bw. Semih Yaran akimuonesha Kamishna Jenerali wa Magereza, CGP- John Casmir Minja(wa pili kulia) maeneo mbalimbali ya mradi huo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...