KAMPUNI ya Simu Tanzania (TTCL) imesema itaendelea na utekelezaji wa kuboresha miundombinu ya mtandao wake wa simu za mezani, mkononi pamoja na huduma za data ili kutoa huduma iliyo bora zaidi kwa wateja wake na kufikia kiwango cha hali ya juu katika kutoa huduma za Mawasiliano nchini. Kauli hiyo imetolewa mwishoni mwa wiki na Kaimu 
 
Afisa Mtendaji Mkuu wa TTCL, Waziri Waziri Kindamba alipokuwa akizungumza na wateja mbalimbali kwenye hafla ya hitimisho la kilele cha Wiki ya Huduma kwa wateja wa TTCL, 2016 zilizofanyika ndani ya Banda la Maonesho ya Biashara la kampuni hiyo lililopo Viwanja vya Mwalimu Julias Nyerere, Sabasaba jijini Dar es Salaam. Kaimu Afisa huyo wa TTCL, alisema kuwa maboresho ya miundombinu yanayofanywa kwa sasa katika shirika hilo yanaliwezesha kukabiliana na changamoto zilizokuwepo awali na kuwapa wateja weke fursa ya kufurahia huduma mpya na za zamani zinazotolewa kisasa na kwa umahiri mkubwa hivi sasa. 
 
"Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) inaendelea na utekelezaji wa uboreshaji wa miundombinu ya mtandao wa simu za mezani, simu za mkononi na huduma za Data ili tuweze kutoa huduma iliyo bora zaidi kwa wateja wetu na kufikia kiwango cha hali ya juu katika kutoa huduma za Mawasiliano," alisema Waziri Kindamba. 
 
Aidha alifafanua kuwa TTCL inawaahidi wateja wake na taifa kwa ujumla kwamba itaendelea kutoa huduma bora, za uhakika na gharama nafuu katika kutengeneza mazingira mazuri ya kiteknolojia, kwani baada ya mabadiliko watumishi wake wameazimia kuongeza kasi ya kufanya kazi kwa bidii, uadilifu, ubunifu na uzalendo wa hali ya juu ili kwenda sambamba na mahitaji ya sasa na baadaye ya wateja wa sekta ya Mawasiliano.
Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Waziri Waziri Kindamba akizungumza na wateja wa kampuni ya TTCL kwenye hafla ya kilele cha Wiki ya Huduma kwa wateja wa TTCL, 2016 iliyofanyika ndani ya Banda la Maonesho ya Biashara la kampuni hiyo lililopo Viwanja vya Mwalimu Julias Nyerere, Sabasaba jijini Dar es Salaam.
Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Waziri Waziri Kindamba (kulia) akimkabidhi mmoja wa wafanyakazi wa kampuni ya TTCL aliyefanya vizuri katika kutoa huduma kwa wateja. Zoezi hilo lilifanyika juzi kwenye hafla ya hitimisho la kilele cha Wiki,ya Huduma kwa wateja wa TTCL, 2016 zilizofanyika ndani ya Banda la Maonesho ya Biashara la kampuni hiyo lililopo Viwanja vya Mwalimu Julias Nyerere, Sabasaba jijini Dar es Salaam Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Waziri Waziri Kindamba (kulia) akimkabidhi mmoja wa wafanyakazi wa kampuni ya TTCL aliyefanya vizuri katika kutoa huduma kwa wateja. Zoezi hilo lilifanyika juzi kwenye hafla ya hitimisho la kilele cha Wiki ya Huduma kwa wateja wa TTCL, 2016 zilizofanyika ndani ya Banda la Maonesho ya Biashara la kampuni hiyo lililopo Viwanja vya Mwalimu Julias Nyerere, Sabasaba jijini Dar es Salaam.
Meneja Uhusiano wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Nicodemas Thomas Mushi (wa pili kulia) akipata picha na baadhi ya wageni waalikwa kwenye hafla ya kilele cha Wiki ya Huduma kwa wateja wa TTCL, 2016 iliyofanyika ndani ya Banda la Maonesho ya Biashara la kampuni hiyo lililopo Viwanja vya Mwalimu Julias Nyerere, Sabasaba jijini Dar es Salaam. Wa pili kushoto ni Ofisa Uhusiano wa TTCL, Edwin Mashasi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...