KATIBU Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Prof. Elisante Ole Gabriel anatarajiwa kufungua kongamano kuhusu mabadiliko ya mifumo ya uendeshaji katika klabu za soka nchini.
 
Kongamano hilo linatarajiwa kufanyika Jumamosi Oktoba 22, mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuhusu mifumo ya kiuendeshaji ambayo klabu kongwe nchini za Simba na Yanga zipo mbioni kuingia na limeandaliwa na Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA).
 
Kongamano hilo litaanza saa nne na nusu asubuhi na litarushwa live (mubashara) na kituo cha televisheni cha Azam kupitia chaneli yake ya Azam Two.Dhamira kubwa ya kongamano hilo ni kupata maoni ya kitaalamu kuhusu mifumo hiyo, ambapo Simba ipo mbioni kuingia mambo ya hisa, wakati Yanga utaratibu wa kukodishwa.
 
Baadhi ya mambo yatakayojadiliwa ni namna ya kuendesha klabu za soka kibiashara, uwekezaji, mambo ya hisa na masuala ya uthamini kukiwa na watalaamu kutoka taasisi mbalimbali nchini.
 
Pia kutazungumzwa umuhimu wa mabadiliko katika klabu hizo na harakati za kuzibadili zilivyoanza miaka ya nyuma na matokeo yake yalivyokuwa.
 
Lengo ni kujadili kitaalamu bila ushabiki wa namna yoyote kwani nia ni kujenga na kuimarisha soka na michezo kwa ujumla hapa nchini na ndiyo sababu tumealika wataalamu wa kada mbalimbali, viongozi wa zamani wa soka kwa tofauti na baadhi ya wadau wa soka.
 
Nawasilisha,
 
Amir Mhando
Katibu Mkuu TASWA
21/10/2016

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...