11-05-1970- 24-10-1999
DAFROSA KWEKA MSENGI
Leo umetimiza miaka kumi na saba
(17) tangu ulipoitwa mbinguni kwa BABA.
Kweli ua zuri limerudi kwenye
Bustani ya Eden. Hatuna cha kusema, tumebaki kushukuru tuu maana imeandikwa
tushukuru kwa kila jambo.
Tunakumbuka sana Upendo na
Ushirikiano, Uchapakazi na uzuri uliokuwa nao. Kweli ulikuwa mfano wa kuigwa,
hata kazini kwako wanakukumbuka. Dfrosa, tupo kama ulivyotuacha ila umebahatika
kuwa na mjukuu mmoja na tumempa jina lako kama ukumbusho. Imani yetu ni kuwa
ipo siku wote tutakutana tena paradise na kufurahi tena pamoja.
Unakumbukwa sana na mumeo mpendwa DR. IBRAHIM MSENGI,mwanao wa pekee Jesca, nduguzo JANE,FESTO,EUGENIA, ELIZABETH,CECILIA na THADEI, shangazi yako mpendwa SR. DEVOTHA KWEKA CDNK,Wajomba,Mashemeji na Mawifi wa kwa BASI wote,
WAKWEKA wote wa NURUMU kina MSENGI wote na MKALAMO – SINGIA,
Wafanyakazi wa idara ya fedha za kigeni- Benki kuu, Majirani wa TEMEKE – MIKOROSHINI na TABATA,ndugu,Jamaa,
na Marafiki wote.
“RAHA YA MILELE UMPE Eee Bwana………………………………….”
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...