OMUTWALE Paschal Rutaihwa Kakiziba
13 JULAI 1935 – 28 OKTOBA 2004

Baba yetu mpendwa umetimiza mwaka wa 12 tangu ulipotwaliwa na Bwana. Picha yako inatukumbusha uwepo wako tulipokuwa sote hapa duniani, na hasa ukarimu, upendo, upole, uchangamfu na wingi wa busara.

Ni vigumu kukubali kwamba haupo nasi lakini hatuna budi kuamini kwamba uko nasi kiroho kwa vile tunaye Mungu ambaye anaendelea kututia nguvu kila iitwapo leo. Busara zako na ucheshi wako vinazidi kutuimarisha kila siku na tunaendelea kuzingatia maneno yako uliyokuwa ukihimiza juu ya kuwa na upendo na umoja katika familia huku tukiendelea kumtumaini Mungu wetu ambaye amekuita kwake.

Mke wako Mary-Hilda Kakiziba, rafiki yako Galita, watoto wako, wajukuu, wakwe zako, dada zako, kaka zako na wadogo zako, ndugu, marafiki na majirani wanakosa ucheshi na ushauri wako na wanakukumbuka daima. MISA YA KUMBUKUMBU ITAFANYIKA JUMAPILI, OKTOBA 30, 2016, SAA 3 ASUBUHI KWENYE KIGANGO CHA MT. ANTHONY WA PADUA, BOKO, DSM.

Tumaini letu linajengwa na neno lisemalo: ”Umevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo umeumaliza na imani umeilinda” (2Tim. 4:7) Tunakuomba Ee Bwana uendelee kuipumzisha roho yake mahali pema peponi, AMEN.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...