Na Vero Ignatus, RSA Arusha. 

Mabalozi wa usalama wa barabarani (Road Safety Ambassadors - Arusha) wamesherehekea sikukuu ya kuzaliwa ya Kamanda Mohammed Mpinga jijini Arusha.  Hafla hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa Milestone Park -Sakina , imeandaliwa na kamati ya (RSA -Arusha) chini ya mwenyekiti wa mkoa Bi. Stella Rutaguza na kuhudhuriwa na wajumbe wa( RSA - Arusha)  "Kwakweli mmenistua jamani sikutegemea kama mmeniandalia jambo kubwa kama hili ,nilijua nakuja kukutana tu na mabalozi ili kufahamiana na kuongelea maswala yetu ya usalama barabarani "alisema Mpinga. 

DCP Mpinga mbaye yupo kikazi jijini Arusha alikutana na mabalozi wa usalama barabarani,kwa lengo la kuongelea na kujadili maswala ya usalama barabarani na mabalozi hao,ambao kazi yao kubwa ni kuelimisha jamii,kukemea na kuripoti matukio yanayoathiri usalama barabarani,na kushawishi mabadiliko ya tabia ,sheria na sera. 

Amezungumzia changamoto iliyopo kwa sasa kwa utoaji wa risiti pale dereva anapotakiwa kulipa faini kutokana na makosa yanayofanyika barabarani,amesema kuwa mfumo huo wa kieletroniki tayari umeshaanza kutumika jijini Dar-es-salaam na hivi karibuni mfumo huo utaanza kutumika katika mikoa sita iliyopewa kipaumbela kabla ya mwaka huu kumalizika.
Kamanda Mohamed Mpinga akipokea "Birthday Surprise Cake " kutoka kwa Mwenyekiti wa RSA -Arusha Bi. Stella Rutaguza katika hafla ya Sikukuu ya kuzaliwa kwake (Mpinga ) iliyoandaliwa na Mabalozi wa Usalama Barabarani na Kufanyika katika ukumbi wa Milestone Park, Sakina Jijini Arusha, 30/10/2016. PICHA NA GADIOLA EMANUEL
Kamanda Mohamed Mpinga akikagua "Birthday Surprise Cake " aliyopewa na Mwenyekiti wa RSA -Arusha Bi. Stella Rutaguza katika hafla ya Siku ya kuzaliwa kwake iliyoandaliwa na Mabalozi wa Usalama Barabarani na Kufanyika katika ukumbi wa Milestone Park, Sakina Jijini Arusha, 30/10/2016.
Katibu wa RSA - Arusha Bw. Gadiola Emanuel akigonga Cheers na Kamanda Mohamed Mpinga katika hafla ya Siku ya kuzaliwa kwake iliyoandaliwa na Mabalozi wa Usalama Barabarani na Kufanyika katika ukumbi wa Milestone Park, Sakina Jijini Arusha, 30/10/2016.
Kamanda Mohamed Mpinga akipata picha ya pamoja na Mabalozi katika hafla ya Siku ya kuzaliwa kwake (Mpinga ) iliyoandaliwa na Mabalozi wa Usalama Barabarani na Kufanyika katika ukumbi wa Milestone Park, Sakina Jijini Arusha, 30/10/2016.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...