Na Humphrey Shao,Globu ya Jamii.

Wanamuziki mahiri wa Muziki wa Taarab, Khadija Kopa,Mwanahawa Ally na Kahadija Yusufu, wanatarajia kuwaburudisha wakazi wa  mji kasoro bahari (Morogoro)  katika tamasha la Muziki litakalokwenda sambamba na zoezi zima la uchangiaji damu.

Akiwatambulisha wasanii hao mapema jijini Dar es Salaam leo Mratibu wa Tamasha hilo ,Hamis Mkongowale(Kajumulo), amesema kuwa tamasha hilo linalenga la kuihamasisha jamii katika suala zima la uchangiaji damu,ili kuokoa maisha ya wenye uhitaji wa damu, hasa wakina Mama na watoto ambao hupoteza damu nyingi wakati wa kujifungua.

"Pamoja na yote haya kutakuwa na maonesho ya uuzaji wa bidhaa mbalimbali kutoka kwa wadau na wajasilimali, hivyo zoezi hili la uhamasishaji litaanza siku tano kabla ya Tamasha husika,ili wananchi wapate huduma husika kwa kukusanya damu kwa wingi kwa ajili ya kuokoa maisha ya Watanzania wenzetu"amesema Kajumulo.

Aliongeza kuwa tatizo la kuona jamii inapoteza maisha kutokana na ukosefu wa damu ni aibu kwa nchi kama hii yenye wakazi zaidi ya milioni 25.

Kwa upande wake gwijinwa muziki wa Taarab nchini Khadija Kopa aliwaomba wakinamama na wakzi wa morogoro wajitokeze kwa wingi siku ya Tamasha hilo hili waweze kufanikishamkuokoa maisha ya wanawake wenzao.
Mwanamuziki mkongwe wa Muziki wa Taarab nchini Khadija Kopa akizungumza na waandishi wa Habari juu ya uwepo wake katika Tamasha la muziki na uchangiaji damu Desemba 25 Mkoani Morogoro.
Mwenyekiti wa Asasi ya Tegemeo Arts na mratibu wa Tamasha hilo Hamis Mkongowale (Kajumulo) Katikati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu namna tamasha hilo litakavyofanyika.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...