MAHAFARI ya tisa ya Wanafunzi wa shule ya mchepuo wa Kiingereza ya Heritage (Heritage English Medium School) jinsi ilivyofana jijini Dar es Salaam leo.

  Wanafunzi wa Shule ya English Medium ya Heritage iliyopo Banana Ukonga jijini Dar es Salaam wa wakiwa wamesimama kwa ukakamavu wakati wa mahafari ya wanafunzi wa shule hiyo wanaohitimu masomo yao ya Darasa la Saba katika shule hiyo.
 Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala, Msongela Palela akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo wakati wa Mahafari ya tisa ya  Darasa la Saba katika shule ya mchepuo wa Kiingereza ya Heritage (Heritage English Medium School) mara baada ya kutembelea maonesho ya masomo mbalimbali ya wanafunzi hao.
Amewapongeza walimu wa shule hiyo kwa kuwafundisha watoto hao hasa watoto wa darasa la awali katika shule ya mchepuo wa Kiingereza ya Heritage (Heritage English Medium School) hasa katika taaluma pamoja na kuwafundisha watoto hao kuwa na hofu ya Mungu.

Amesema kuwa serikali ya awamu ya tano ikiwa na sera ya Kusimamia na Kuimarisha elimu katika shule za awali katika shule zote za msingi kuwa na madarasa ya awali ili kuwezesha kutoa watoto wakiwa na uelewa bora.

Amesema katika Manispaa ya Ilala ina shule msingi za serikali 121, Shule za Binafsi za msingi 89 na shule za awali za serikali 99 pamoja na shule za binafsi za awali 84.
 Mwalimu Mkuu wa shule ya mchepuo wa Kiingereza ya Heritage (Heritage English Medium School), Kebaso Elia akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo wakati wa mahafari ya tisa ya Darasa la Saba katika shule hiyo.
Amewaomba Wizara ya elimu, sayansi na Teknologia iwapitishe waandishi wa vitabu vya kiada na ziada  ili kusitokee mkanganyiko katika ufundishaji wa watoto na kuwa na utofauti kati ya vitabu.
 Wahitimu wa shule ya mchepuo wa Kiingereza ya Heritage (Heritage English Medium School) wakiingia ukumbini jijini Dar es Salaam leo katika mhafari ya tisa ya shule hiyo.
Picha na Avila Kakingo, Globu ya Jamii.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...