Mke wa Rais Mama janeth Magufuli leo amehudhuria kwenye msiba wa shemejie Rais Mstaafu Dkt.Jakaya Kikwete marehemu Mariam Ramadhani Saburi aliyefariki Dunia katika hosptali ya Taifa muhimbili jijini Dar es salaam kwa kusumbuliwa na maradhi ya miguu. 
Marehemu, ambaye ni Mama Mdogo wa Mbunge wa Jimbo la Chalinze Mhe. Ridhiwani Kikwete alifariki Jana asubuhi hospitalini hapo baada ya Kulazwa Kwa muda wa mwezi mmoja akisumbuliwa na maradhi ya hayo. Mazishi hayo yamefanyika katika makaburi ya Mwanakalenge,wilayani Bagamoyo mkoani Pwani na kuhudhuliwa  na mamia ya waombolezaji wakiwemo viongozi mbalimbali wa vyama vya siasa na serikali. Marehemu Bi Mariam ameacha watoto watatu na wajukuu wawili.
Inna lillahi wa inna ilayhi raji'un








 Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli (kulia) akilakiwa na Mke wa Rais Mstaafu Mama Salma Kikwete alipowasili kwenye msiba wa Marehemu Mariam Ramadhani Saburi, shemeji yake Rais Mstaafu Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete aliyefariki jana na kuzikwa huko Bagamoyo leo  Oktoba 10, 2016
Mwanga, 
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli (kulia) akifariji wana familia wa Bibi Maguno Binti Athumani ambaye ni  mkwe wa Rais Mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete kwenye msiba wa shemejie  (Rais Mstaafu)   Marehemu Mariam Ramadhani Saburi   aliyefariki jana na kuzikwa huko Bagamoyo leo Oktoba 10, 2016

 Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli (wa tatu kushoto) akiwa na  Mke wa Rais Mstaafu Mama Salma Kikwete (kulia) akimfariji Bi Maguno Binti Athumani ambaye ni mkwe wa Rais Mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete kwenye msiba wa shemeji  yake (Rais Mstaafu)  Marehemu Mariam Saburi aliyefariki jana na kuzikwa huko Bagamoyo leo Oktoba 10, 2016
 Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akimpa mkono wa pole Rais Mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete kwenye msiba wa shemeji  yake (Rais Mstaafu) marehemu Mariam Ramadhani Saburi  aliyefariki jana na kuzikwa  huko Bagamoyo leo Oktoba 10, 2016
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli (kulia) akiwafariji watoto wa  shemejie Rais Mstaafu Mhe Jakaya Mrisho Kikwete, Marehemu Mariam Ramadhani Saburi,    aliyefariki jana na kuzikwa huko Bagamoyo leo Oktoba 10, 2016.






Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...