Na Ramadhan Ali/Maelezo Zanzibar
Mamlaka
ya Usafiri wa Baharini Zanzibar (ZMA) imekanusha tuhuma zinazotolewa
kuwa imesajili meli za Korea Kaskazini kinyume na Azimio la Baraza la
Usalama la Umoja wa Mataifa lililopitishwa mwezi Machi mwaka huu za
kuzikatalia usajili Kampuni za meli za nchi hiyo.
Akizungumza
na Waandishi wa Habari, Mkurgenzi Mkuu wa ZMA Abdalla Hussein Kombo
amesema tuhuma hizo zilizotolewa na Mkurugenzi wa Habari na Uchambuzi wa
Taasisi ya NK News kupitia Jarida la NK Pro la Mjini Seoul, Korea
Kusini sio za kweli.
Amesema
ZMA baada ya kupata taarifa ya Azimio hilo iliunda Kamati ya wataalamu
kulifanyia uchambuzi na kutoa mapendekezo kwa Mamlaka juu ya hatua za
kuchukuliwa."Azimio
hilo limetaja majina ya meli 31 za Korea Kaskazini ambazo nchi zote
wanachama wa Umoja wa Mataifa, ikiwemo Tanzania, inazitaka kuzifutia
usajili au kutozisajili," alisema Mkurugenzi Mkuu ZMA.
Aliongeza
kuwa ZMA ilifanya uhakiki wa meli zote zilizosajiliwa na Mamlaka hiyo
na orodha ya meli zilizoainishwa kupitia Azimio hilo na kubaini kuwa
meli moja yenye jina la First Cleam ilikuwa imesajiliwa kabla ya vikwazo
vya usajili wa meli za Korea Kaskazini lakini ikaamua kuifutia usajili.
Amesema
kuanzia wakati huo, Mamlaka haijawahi kusajili meli yeyote ambayo
ilikuwemo katika orodha iliyotolewa na Umoja wa Mataifa na imekuwa
ikichukua tahadhari kubwa katika usajili wa meli.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri Baharini Zanzibari (ZMA) Abdallah Hussein Kombo akizungumza na waandishi wa Habari kukanusha tuhuma za kusajili Meli za Korea ya Kaskazini kinyume na Azimio la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
Waandishi wa Habari wakimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Baharini Abdallah Hussein Kombo wakati alipokutana nao Ofisini kwake Malindi .
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji Zanzibar Mustafa Aboud Jumbe akitowa ufafanuzi wa masuala yaliyoulizwa na Waandishi wa Habari katika Mkutano huo. (Picha na Miza Othman Habari Maelezo Zanzibar).
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...