Mkurugenzi Mkazi wa Marie Stopes, Anil Tambay (katikati) akiongea na waandishi wa habari kuelezea juu ya maadhimisho ya miaka 40 kwa kutoa huduma bure za uzazi wa mpango na uchunguzi wa kansa ya mlango wa kizazi kama maadhimisho ya miaka 40 ya Marie Stopes International. Maadhimisho hayo yanatarajia kufanyika Novemba 2-4, 2016 kwenye kliniki na hospitali zake zote nchini Tanzania.
Marie Stopes Tanzania itatoa huduma za uzazi wa mpango na uchunguzi wa kansa ya mlango wa kizazi bure kuanzia tarehe 2 hadi 4 Novemba kwenye kliniki na hospitali zake zote nchini kama sehemu ya kuadhimisha miaka 40 ya Marie Stopes International, na hivyo kuongeza idadi ya akina mama ambao wamewezeshwa kuwa na maamuzi juu ya mustakabali wa maisha yao wa kupata watoto kwa utashi na si kwa kubahatisha.

Marie Stopes Tanzania ni sehemu ya Marie Stopes International, shirika la kimataifa linalojihusisha na kutoa huduma za afya ya uzazi na lilianzishwa mwaka 1976. Katika wiki inayoanzia Oktoba 31, tutakuwa tuaadhimisha miaka 40 tangu kuanzishwa kwa Maries Stopes International.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...