Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masaun aagiza Jeshi la Magereza kuzidi kuboresha viatu vinavyotengenezwa na kiwanda chao ili kujipatia soko kubwa ndani ya nchi na nje. 
Hayo aliyasema jana kwa wakuu wa Gereza la karanga na viongozi wa kiwanda hicho alipofanya ziara yake ya siku moja katika kiwanda cha viatu kilichopo katika gereza hilo, mkoani Kilimanjaro
Aidha, Naibu Waziri huyo alisisistiza Jeshi hilo kutekeleza agizo la Rais John Magufuli kuhakikisha majeshi yote nchini yanatumia viatu vinavyozalishwa na Jeshi la Magereza, hivyo ni muhimu kuendelea kuzalisha bidhaa zilizo bora zaidi
Haiingii akilini maofisa wa majeshi mbalimbali nchini kuagiza viatu nje ya nchi wakati viwanda vya ndani vinauwezo wa kuzalisha viatu bora zaidi vinavyodumu kwa muda mrefu kuliko vinavyoagizwa kutoka nje ya nchi, alisema Masauni.

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni akijionea kiatu aina ya Safari buti kinachozalishwa na Kiwanda cha Karanga kilichopo Mkoani Kilimanjaro wakati akiwa katika ziara ya kikazi ya siku moja kiwandani katika Mkoa huo. Masauni amesisitiza kiwanda hicho kuzalisha bidhaa bora zaidi ili kuteka soko kubwa zaidi pamoja na kutekeleza agizo la Rais Magufuli kuhakikisha majeshi yote nchini yanatumia viatu vinavyozalishwa na Jeshi hilo. Kulia ni Mkuu wa Kiwanda hicho Mrakibu Msaidizi, Michel  Minja na kushoto ni Ali Jambaraga Fundi Mkuu. 
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni akiangalia kiatu kilichokuwa tayari kuvaliwa kilichotengenezwa katika kiwanda cha Karanga kilichopo Gereza Kuu la Karaga mkoani Kilimanjaro. Naibu Waziri huyo amesisitiza Jeshi hilo kuzidi kutengeneza bidhaa bora zaidi za viatu ili kuhakikisha wanapata soko kubwa ndani nan je ya nchi., kulia ni Kamishan Msaidizi Mwandamizi wa Mkoa wa Kilimanjaro, Wilbroad Mutafungwa aliye aambatana nae kwenye ziara hiyo. 
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masaun (aliyevaa koti) akitoa maelekezo kwa Wakuu wa Gereza la Karanga na kiwanda cha Viatu kilichopo gerezani hapo. Masauni amelitaka jeshi hilo kuzidi kutoa bidhaa bora ili kuendelea kuteka soko kubwa ndani nan je ya nchi. 

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...