NA VICTOR MASANGU, RUFIJI.

MBUNGE wa jimbo la rufiji Mohamed Mchengerwa ameahidi kuvisadia vikundi mbali mbali vya wakinamama wajasiriamali kwa lengo la kuweza kuwainua kiuchumi na kuweza kuinua mitaji waliyonayo ili kuondokana na janga la umasikini na kuwa tegemezi.

Mchengerwa ameyasema hayo wakati wa ziara yake ya kikazi kwa ajili ya kuwatembeea wananchi wa jimboni kwake kwa ajili ya kuweza kubaini changamoto mbali mbai zinazowakabili kwa lengo la kuweza kuzitafutia ufumbuzi.

Alisema kuwa katika jimbo lake la rufiji kuna vikundi mbali mbali vya ujasiriamali hivyo atajitahidi kwa hali na mali kuvisaidia kuviwezesha fedha ambazo itaweza kuwa ni mkombozi mkubwa kaatika shughuli zao za kila siku na kuleta mabadiliko chanaya ya kimaendeleo.

“Mimi kama mbunge wa jimbo la rufiji wananchi mmenipa dhamana kubwa ya kuwatumikia hivyo kwa upande wangu nitahakikisha yale yote ambayo nimewea kuwaahidi wakati wa kampeni nitayafanyia kazi kwa vitendo, na ninahitaji wakinamama wote mjiunge katika vikundi ili iweze kuwa rahisi katika kuwasaidia kuliko mtu mmoja mmoja,”alisema Mchengrwa.

Aidha aliongeza kuwa ana imani endapo vikundi hivyo vya wakinamama vikiwezeshwa vitaweza kupiga hatua kubwa ya kuweza kujiajiri wao wenyewe na kuendesha biashara zao ambao zitaweza kuwapataia kipato amabcho kitaweza kusaidaia katika kuendesha familia zao kuliko ya kuwa na tabia ya kuwa tegemezi kwa watu wengine.

Alisema kuwa japo anatambua wananchi wa jimbo lake wanakabiliwa na changamoto mbali mbali lakini kwa kushirikiana na serikali ya awamu ya tano atashirikiana nayo bega kwa bega kwa lengo la kuweza kuleta maendeleo makubwa katika Wilaya ya Rufuji.

Aidha katika hatua nyingine Mchengerwa katika ziara yake hiyo aliweza kukitembelea kikundi cha wakinamama wajasiriamali katika kijiji cha mloka na kukikabidhi kiasi cha shilingi laki tano kwa lengo la kuweza kukuza mtaji wao pamoja ana kujiendeleza zaidi katika kukuza biashara zao wanazozifanya kila siku.

Pia mbunge huyo aliwahimiza wakinamama wa wilayani Rufiji kuhakikisha fedha hizo zilizotolewa kwa ajili ya kikundi zinatumika vizuri bila ya kuwa na ubaguzi wa aina yoyote na badala yake zitumike kwa manufaa ya wanachama wote ambao wanatarajia kujikwamua kiuchumi na kuweza kuondokana na tatizo la umasikini.
Mbunge wa jimbo Rufiji Mohamed Mchengerwa kulia akimkabidhi mmoja wa viongozi wa kikundi cha wakinamama wajasiriamali katika kijiji cha Mloka cheki ya kiasi cha shilingi laki tano kwa ajili ya kuwasaidia kuwainua kiuchumi na kukuza mtaji wao
Mbunge wa jimbo la Rufiji Mohamed Mchengerwa wa kati kati akiwa katika picha ya pamoja na badhi ya wakinamama baada ya kufanya ziara yake ya kuwatembelea kwa ajili ya kuweza kubaini chanagamoto zao zinazowakabili.(PICHA NA VICTOR MASANGU)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...