Afisa Mtendaji wa Kata ya Mburahati Jijini Dar es salaam ametakiwa kusimamia kwa uaminifu mapato ya soko Mburahati ili kuimarisha mapato ya Manispaa hiyo ambayo yataimarisha uboreshaji wa huduma mbalimbali kwa wananchi.
Agizo hilo limetolewa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo wakati alipofanya ziara sokoni hapo kwa lengo la kujionea hali halisi ya soko pamoja na hali ya ukusanyaji wa mapato.
Sambamba na agizo hilo pia Mkurugenzi amemtaka Afisa Mtendaji huyo kwa kushirikiana na kamati ya soko Kuandaa orodha ya majina ya walipaji wote pamoja na kiasi wamachotakiwa kulipa, kutolewa namba pamoja na kuwepo na orodha ya kiasi kinachotakiwa kukusanywa kutoka katika maduka hayo, Kutoa mapendekezo mapya ya viwango vya tozo, na kuwepo na jina la kila mmiliki wa meza sokoni hapo na kiasi cha ushuru anacholipa.
MD Kayombo ametoa siku tano kwa Afisa Mtendaji huyo kwa kumtaka Kuwasilisha orodha ya watu wote wanaodaiwa tozo na kodi katika soko na vibanda pamoja na muda wanaodaiwa sambamba na Kutengeneza data base ya wafanyabiashara wote katika soko hilo.
Pamoja na ukaguzi huo Mkurugenzi alipata maelezo juu ya ukusanyaji mapato katika soko la Mburahati lililopo pembeni ya jengo la soko linalojengwa. Akisomewa taarifa ya soko hilo na katibu wa soko Ndg Fikiri Pazi alisema kuwa wenye meza hulipa kiasi cha shs 200 kwa siku na wenye vibanda (maduka)hulipa shs21000 kwa mwezi viwango ambavyo wamekuwa wakilipa tangu kuanza kwa soko hilo mwaka 1982.
Mkurugenzi hakuridhika na viwango hivyo kwa ni ni viwango vilivyopitwa na wakati kutokana na hilo ameagiza tozo hizo ziangaliwe upya na walete mapendekezo ya viwango vipya ambapo menejimenti ya Manispaa itavipitia na kulinganisha na mapendekezo ya viwango vya menejimenti na kisha kufanya maamuzi ya viwango vipya.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...