Na Woinde Shizza,Arusha

Mkurugenzi wa halmashauri ya jiji la Arusha, Athumani Kahamia ametoa ufafanuzi kuhusu tuhuma ya matumizi mabaya ya fedha kiasi cha sh, 500 milioni zilizotengwa kwa ajili ya ujenzi wa jengo la utawala katika halmashauri ya Kaliua na kusema kwamba fedha hadi anahamishwa fedha hizo hazikuwahi kuletwa katika halmashauri hiyo kutoka serikali kuu.

Hivi karibuni kumekuwa na tuhuma mbalimbali zinazosambaa kwenye mitandao ya kijamii nchini ambapo Kahamia anatuhumiwa kutumia kiasi hicho cha fedha zilizotengwa kwa ajili ya ujenzi wa jengo la utawala katika halmashauri ya Kaliua wakati akiwa mkurugenzi wa Kaliua kabla ya kuhamishiwa jijini Arusha.

Akihojiwa na mwandishi Wa Habari hizi Kahamia alisema kwamba aliripoti mnamo febuari 2015 katika halmashauri hiyo na kukuta ujenzi wa jengo la utawala ukiendelea ambapo katika bajeti ya halmashauri ya Kaliua mwaka wa fedha 2015/16 waliomba fedha hizo kwa ajili ya kukamilisha ujenzi huo katika awamu ya kwanza lakini serikali haikuleta pesa hizo.

Alisema ya kwamba lakini pamoja na kutenga bajeti ya fedha hizo halmashauri hiyo haikupokea kiasi hicho kutoka serikali kuu na kusisitiza kwamba hadi anaondoka Kaliua fedha hizo hazikuwahi kuzipokea.

"Hadi tarehe 30 juni mwaka huu hizo fedha tulikuwa bado hatujazipokea mpaka leo tunavyoongea hizo fedha hazijapokelewa taarifa kwamba nimezitafuna zinalenga kunichafua "alisema Kahamia

Hatahivyo, alifafanua tuhuma kwamba tayari ameandikiwa barua ya kurudishwa Kaliua ili kujibu tuhuma zinazomkabili na kusema si kweli kwani hadi sasa hajapokea barua yoyote wala wito kutoka mamlaka yoyote kumtaka arudi kujibu madai hayo.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...