Mkuu wa Wilaya ya wa Wilaya ya Kongwa, Deo Ndejembi  akisaidiana na wananchi kuvuluga bustani zilizopo karibu na vichoteo vya maji.
DC wa Wilaya ya Kongwa MH Deo Ndejembi Amelifanya zoezi hilo akiwa na Kamati yake ya Ulinzi na Usalama, Mkuu wa Wilaya Ndejembi ameamua kufanya zoezi lakutifua Bustani hizo Baada ya Wananchi wanaoishi karibu na vichoteo hivo kuamua kulima Bustani za Mboga mbona wakiwa wanatumia Maji ya Bomba ambayo hupaswa kusukumwa kujaza Tanki Kubwa.


Wananchi hao wamekuwa wanafungulia Maji ya Bomba nakumwagika chini ili kuelekea katika Bustani Zao, Hufanya hivo nyakati za usiku Muda ambao Pampu inasukuma Maji kuelekea Tanki la Mjini ili Lijae na Kuhudumia Wakazi wa Mjini Kongwa.

Kutokana na kutokujaa Tanki Hilo la Mjini kwa sababu ya wananchi hao kufungulia Maji nakumwagika nyakati za usiku basi Kongwa kumekuwa na Shida Kubwa ya Maji.

DC aliongozana na DAS wake Ndg Audiphace Mushi Ambae alishiriki kikamilifu ktk zoezi lakutifua Bustani hizo, Akiwamo Mkurugenzi Mpya wa Mamlaka ya Maji Ndg Hamisi Ally Anaekaimu nafasi hiyo  Baada ya aliekuwa Mkurugenzi mamlaka hiyo kumsimamishwa na DC Ndejembi wiki moja ilopita.

Pia Aliongozana na Mshauri wa Mgambo Sajent Taji Paul Nkwabi, Pia Alikuwapo Kaimu Afisa Tawala Ndg Denis Semindu nk....

Kabla yakuanza zoezi lakuvuruga Bustani hizo DC Ndejembi aliamuru wananchi Kuchuma mbonga zilizokuwapo ktk Bustani hizo, Pia Kuchukua Maji ambayo yalikiwa yamehifadhiwa ktk Bustani hizo kwa ajili yakumwagilia.
Lakini Pia Walifanya zoezi lakutafuta Mpira ambao Hutumika kuonganisha ktk Bomba nakupeleka shambani, Wamiliki wa Bustani hizo walikimbia na kuficha mipira hiyo.

Vichoteo hivo Viko Kijiji cha Ibwaga ambapo viliwekwa mahususi kusaidia Wanakijiji wa Vijiji vya karibu, Vichoteo hivo vilitobolewa katika Bomba Kuu ambao linaelekea Mjini na Walipewa Muda wakutumia Kuanzia Asubui mpaka Jioni saa 12 kisha wafunge na Kuacha Pampu isukume Maji Mjini ili kujaza Tanki kubwa, cha ajabu nikuwa wananchi hao wamekuwa hawafungi Mabomba hayo Usiku bali huendelea kuchota maji na wengine kufungulia kumwagilia Bustani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...