Na
Theresia Mwami TEMESA Geita.
Mkuu
wa Wakala wa Ufundi na Umeme TEMESA Dkt. Mussa Mgwatu amewataka watendaji wake
katika vituo vyote vya TEMESA nchini kuanza kujenga mazingira ya kujitegemea na
kuondokana na fikra za kutegemea fedha kutoka Serikalini.
Agizo
hilo limetolewa na Mtendaji huyo alipotembelea karakana ya TEMESA iliyopo
mkoani Geita na kujionea kazi zinazofanywa na karakana hiyo na kuagiza watendaji
wake kutafuta mbinu mbadala ya kuzalisha mapato ili waweze kujiendesha wenyewe.
“Naomba
muanze mikakati ya kufanya kazi kwa kasi na ubora na kuongeza ubunifu ili
kuhakikisha kituo kinakusanya mapato ya kutosha kuweza kujiendesha kwa kuwa serikali
hapo baadae haitaendelea kutoa ruzuku kwa taasisi zake zote zinazozalisha”
alisisitiza Dkt. Mgwatu.
Mtendaji
Mkuu huyo amemuagiza Meneja wa TEMESA Geita kuhakikisha anafanya matengenezo
sehemu ya kutengenezea magari iliyopo kituoni hapo, kuwapa mikataba watumishi wote
wasio na ajira za kudumu, kuhakikisha watumishi wanapata vitendea kazi
kulingana na mahitaji ya kada zao, kufuatilia kwa karibu wadaiwa sugu wa kituo,
na kuhakikisha madeni yaliyopo sasa yanalipwa pamoja na kuongeza uzalishaji wa
kituo
hicho.
Kwa
upande wake Meneja wa TEMESA Mkoa wa Geita Mhandisi Gilly Chacha ameeleza changamoto
zilizopo kuwa ni uchakavu wa karakana na vifaa vya kazi pamoja na uwepo wa
madeni sugu wanazozidai Ofisi ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Geita, Halmashauri ya
Wilaya ya Chato na Mbongwe pamoja na ofisi ya Mkurugenzi wa Mji wa Geita.
“Mtendaji
tunakuahidi kuanza kutekeleza agizo lako la kuzalisha mapato zaidi ili
tujitegemee na kutotegemea ruzuku kutoka Serikalini kwa kuwa wabunifu na
kujituma katika kazi na kukusanya madeni yote tunayodai” alisema Mhandisi Gilly
Chacha.
Aidha
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme TEMESA Dkt. Mussa Mgwatu amemtaka
Meneja wa TEMESA Geita kumpatia taarifa za ufuatiliaji wa madeni ya wadaiwa
sugu na taarifa ya mapato yaliyokusanywa na kituo kwa mwaka wa fedha 2016/2017
ili kujua pato halisi la kituo.
Mtendaji
Mkuu wa TEMESA Dkt. Mussa Mgwatu yupo katika ziara ya kikazi Kanda ya Ziwa na
atatembelea vituo vya TEMESA vilivyopo ili kubaini changamoto na kujionea
utendaji kazi wa vituo hivyo na sasa yupo Mkoani Geita.
Mtendaji Mkuu wa TEMESA Dkt. Mussa Mgwatu (kulia) akisikiliza taarifa ya Meneja wa TEMESA Geita Mhandisi Gilly Chacha (Kushoto) alipotembelea kituoni hapo
Mtendaji Mkuu wa TEMESA Dkt. Mussa Mgwatu (kulia) akikagua sehemu ya kutengenezea magari katika karakana ya TEMESA Geita alipotembelea kituoni hapo (aliyevaa miwani) ni Meneja wa TEMESA Geita Mhandisi Gilly Chacha.
Watumishi wa karakana ya TEMESA Geita wakimsikiliza Mtendaji Mkuu wa TEMESA Dkt. Mussa Mgwatu (hayupo pichani) alipotembelea kituoni hapo.Picha zote na Theresia mwami TEMESA Geita.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...