Na May samba-MAELEZO.

Mapema mwezi September mwaka huu muswada wa huduma za habari ulisomwa kwa Mara ya kwanza bungeni na kutolewa fursa kwa wadau wa habari kutoa maoni ili kuuboresha.

Takribani miezi miwili sasa imepita tangu wadau walipotakiwa kuusoma na kutoa maoni, lakini cha kushangaza wamekuja na sababu lukuki ikiwamo “ETI” kukosa muda wa kuusoma, Muswada wenye kurasa 28 tu.

Kimantiki wachambuzi wa masuala haya wanasema kuwa muswada huu unahistoria ndefu ya zaidi ya miaka 20 ambapo wadau katika sekta ya habari wamekuwa wakipigania kuipa heshima taalum hii na kuifanya kuheshimika kama fani za aina nyingine nchini.

Kwa kujua, kutojua au kwa makusudi wapo baadhi ya watu walio ndani ya tasnia ya habari na wasio wanatasnia wamekuwa wakivipotosha vifungu muhimu ndani ya muswada huu inawezekana kwa maslahi yao binafsi au kutumika na watu wenye nia mbaya na tasnia hii waliosahau maslahi mapana ya tasnia ya habari nchini.

Akizungumza kwa nyakati tofauti Mkurugenzi wa Idara ya Habari-MAELEZO  Bw. Hassan Abbas amesema lengo la muswada huu ni kuja na sheria itakayokuza na kuimarisha taaluma na weledi katika tasnia ya habari na kuweka mfumo wa usimamizi wa huduma za habari.

Jambo lingine lililoibua mjadala kwenye muswada huu ni kuhusu taaluma kwa waandishi wa habari ambayo imeibua hofu kwamba wanahabari wasiokuwa na kiwango cha elimu kwa ngazi ya shahada watafukuzwa, kuachishwa kazi au kutotambulika kama wanahabari.

Akilitolea ufafanuzi suala hilo Bw. Abbas amesema kuwa waandishi hawapaswi kuwa na hofu kwani kutakuwa na viwango tofauti vya utambuzi katika fani ya habari na pia kutatolewa muda wa miaka mitano kwa waandishi wa habari kujiendeleza.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...