Mkuu
wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (kulia) akipokea Mwenge wa Uhuru kutoka
kwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack (kushoto) katika kijiji cha Wigelekelo
wilayani Maswa ukitokea Kishapu Mkoani Shinyanga.
Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akisoma
taarifa ya Mkoa kwa Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2016, Ndg. George
Mbijima katika kijiji cha Wigelekelo wilayani Maswa mara baada ya kupokea Mwenge
wa Uhuru kutoka Mkoani Shinyanga.
Baadhi
ya wasanii wa Ngoma ya Wagoyangi kutoka Maswa wakitoa burudani kwa kucheza
ngoma wakiwa na nyoka aina ya chatu, mbele ya wananchi wa Wilaya hiyo waliofika
katika mapokezi ya Mwenge wa Uhuru katika kijiji cha Wigelekelo.
Mkuu
wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(kushoto) akimkabidhi Mwenge wa Uhuru Mkuu
wa wilaya ya Maswa, Dkt. Seif Shekalaghe.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...