Mkurugenzi wa Utawala na
Usimamizi wa Rasilimali Watu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Lilian Mapfa akiaga
mwili wa Mwanasheria wa Wizara hiyo, marehemu, Yusta Msoka, ambaye alifariki
wiki iliyopita na mwili wake ulizikwa Mbagala, jijini Dar es Salaam jana. Nyuma
ya Mapfa, ni Mkuu wa Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA)
wa Wizara hiyo, Jane Massawe. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya
Nchi.
Mkurugenzi wa Idara ya Sheria wa Wizara
ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Marlin Komba, Afisa Sheria wa Wizara hiyo, Berious
Nyasebwa wakiaga mwili wa mwanasheria mwenzao wa Wizara hiyo, marehemu, Yusta
Msoka, ambaye alifariki wiki iliyopita na mwili wake ulizikwa Mbagala, jijini
Dar es Salaam jana. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi,
Balozi Simba Yahya (kushoto), Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali
Watu, Lilian Mapfa (kushoto kwa Balozi), Mkurugenzi wa Idara ya Sheria wa
Wizara hiyo, Marlin Komba wakiwa katika hali ya huzuni pamoja na waombolezaji
wengine wakati wa kuaga mwili wa marehemu, Yusta Msoka, ambaye alifariki wiki
iliyopita na mwili wake ulizikwa Mbagala, jijini Dar es Salaam jana.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...