UMOJA wa Wafanyabiashara wa kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya watu wa Congo (DRC)  Bw. Sumael Edward, ametangaza kurejea kwa wafanyabiashara wa nchi hiyo kutumia Bandari ya Dar es Salaam. 
Bw. Edward alisema hayo jijini Dar es Salaam leo alipokuwa akizungumza na Waandishi wa habari katika ukumbi wa iadara ya Habari Maelezo.
“Sisi kwa moyo mmoja tumeamua kurejea Bandari ya Dar es Salaam mara baada ya Baba zetu wote wawili Rais John Magufuli na Joseph Kabila kukubaliana mambo mazuri ambayo sisi kama wafanya biashara tunaona yana tija kwetu katika kukuza umoja wetu kati ya Tanzania na DRC”amesema Edward.
 Aliongeza kuwa kwa sasa wanashukuru mizigo yao kwa sasa haikai bandarini kwa kuchelewa na hakuna ubabaishaji wa kupelekwa bandari pasipokuwa na lazima.
 Alimaliza kwa kusema kuwa kwa sasa wananchi wa DR Congo wote wameanza kurejea Tanzania na biashara zote zitakuwa kama zamani na maduka yote Kariakoo yatapata wateja.
Rais wa Wafanyabiashara wa nchini DR Congo Bw. Sumael Edward akiongea na waandishi wa Habari jijini Dar es salaam. Pembeni yake ni afisa Habari wa Idara ya Habari MAELEZO, Bw. Tiganya Vicent. 
Picha na Habari na Humphrey Shao wa Globu  ya Jamii

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Maneno mazuri humtowa nyoka pangoni. Pongezi za dhati kwa Marais wa pande hizo mbili kwa mazungumzo ya pamoja ikiwa ni katika kudumisha na kujenga uhusiano mzuri wa kimaendeleo khususan katika nyanja za kiuchumi na kibiashara mbali ya uhusiano wa karibu sana wa kiujirani na kindugu uliyopo kati ya Tanzania na DRC. Daima umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...