Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Hanang’ Mkoani Manyara, Bryceson Kibasa akizungumza na wananchi wa Tafara ya Simbay kwenye uzinduzi wa mfuko wa afya ya jamii iliyoboreshwa (iCHF) ambapo alisema wameboresha hospitali ya wilaya hiyo Tumaini ikiwemo dawa kupatikana kwa wingi.
 Meneja wa mfuko wa Taifa wa Bima ya Taifa Nchini (NHIF) Mkoani Manyara, Henry Shekifu akizungumza na wananchi wa Tarafa ya Simbay Wilayani Hanang’ juu ya umuhimu wa kujiunga na mfuko wa afya ya jamii iliyoboreshwa (iCHF) ambapo huduma hizo zitatolewa kwenye zahanati, vituo vya afya na hospitali zote za Serikali ndani ya wilaya pia katika zahanati, vituo vya afya na hospitali binafsi na taasisi za dini zilizo ndani ya wilaya na kusajiliwa.
 Mkuu wa Wilaya ya Hanang’ Mkoani Manyara, Sarah Msafiri Ally akizungumza kwenye uzinduzi wa mfuko wa afya ya jamii ulioboreshwa (iCHF) wilayani hupo ulioratibiwa na ofisi ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Mkoani Manyara na kufanyika katika Kata ya Simbay ambapo wananchi wanapaswa kuchangia shilingi 30,000 na kutibiwa kaya moja yenye watu sita kwa mwaka mmoja.
Mkazi wa Tarafa ya Simbay Wilayani Hanang’ Mkoani Manyara, Stephan Songay akizungumza kwa kuwasisitizia wananchi wa eneo hilo kujiunga na mfuko wa afya iliyoboreshwa iCHF kwa kuchangia shilingi 30,000 na kutibiwa bure kwa mwaka mmoja, kaya moja yenye watu sita, baba, mama na watoto wanne ambao hawajatimiza umri wa miaka 18.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...