Wiki ya kwanza ya mwezi Oktoba hujulikana kama wiki ya huduma
kwa mteja na huadhimishwa duniani kote. Benki ya NMB imeamua kuendelea kusherehekea
huduma kwa mteja kwa mwezi mzima ili kuonyesha jinsi inavyomjali mteja kibiashara,
kimaendeleo pamoja na amani kwa ujumla. NMB imejikita kwenye kutoa huduma bora
zinazofikia malengo ya wateja wa ndani na nje.
Kutana na Meneja Mwandamizi
wa huduma kwa wateja wa NMB, Amanda Feruzi anayetuelezea maoni binafsi
na ya kampuni kuhusu huduma kwa mteja na kwanini ni muhimu kuadhimisha huduma
kwa mteja.
Mimi: Karibu sana Amanda, tuanze kwa
kufahamu jukumu lako ni nini?
Amanda: Jukumu langu ni kutengeneza, kuratibu, kufuatilia na kupima ubora wa
huduma kwenye benki
Mimi: Huduma kwa mteja inamaanisha nini
kwako na kwenye benki kwa ujumla?
Amanda: Binafsi, naamini kwamba huduma kwa mteja
ni kuwaheshimu na kuwajali wateja kwa kutumia weledi kufanikisha mahitaji yao.
Kama shirika – huduma kwa wateja ni jambo la msingi sana hapa NMB na ndio maana
kila siku tunaboresha huduma na bidhaa zetu ili kufanikisha malendo ya wateja
wetu.
Mimi: Kwanini ni muhimu kuwa na wiki ya
huduma kwa mteja?
Amanda: Wateja wetu (wa ndani na nje) ndiyo sababu ya sisi kuwa na mafanikio.
Kwahiyo, tunasherehekea mchango wao na kuwaahidi kwamba TUNAWAJALI kwa kuwa
sehemu ya mafanikio yetu.
Mimi: Ni kitu gani cha muhimu sana cha
kufuata unapokuwa unamhudumia mteja?
Amanda: Kitu cha msingi sana wakati wa kumhudumia mteja ni kuhakikisha
mahitaji na matarajio yake yanafikiwa. Inapotokea kwamba kwa namna moja au
nyingine hatujafikia matarajio ya mteja wetu, tunachukua mrejesho na kulifanyia
kazi suala hilo.
Mimi: Msemo wa “mteja ni mfalme” una ukweli
kiasi gani?
Amanda: Tunaposema mteja ni mfalme, tunarudi palepale kwenye kutilia
msisitizo wa kusherehekea wiki ya huduma kwa mteja. Mteja ni mfalme kwa sababu
ndiye sababu ya sisi kufanikiwa na kuongeza jitihada ili kufanikisha malengo
yake. Mteja anahitaji huduma bora kwenye pesa zake hivyo, ni wajibu wetu
kumsikiliza kwa makini, kumwelewa na kufanikisha mahitaji yake.
Mimi: Kama huduma kwa mteja ingekuwa ni
mnyama, unafikiri angekuwa ni mnyama gani na kwanini?
Amanda: Hilo ni swali zuri lakini gumu pia. Mi nafikiri ningefananisha wiki
ya mteja na tembo. Tembo ni wapole na viongozi wasiotumia mabavu. Hiyo ndio
sababu tembo wenzao huwaheshimu kutokana na uwezo wao wa kutatua matatizo. Hiyo
ni sawa na hhuduma kwa mteja.
Mimi: Ahsante sana kwa kuzungumza nasi kuhusu
huduma kwa mteja na namna mlivyojipanga kuhakikisha kwamba mnatimiza matarajio
ya wateja wenu.
Amanda: Shukrani sana.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...