Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa, ameitaka Bodi mpya ya Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) kusimamia Menejimenti ya Mamlaka hiyo katika Idara ya Utawala na Rasilimali watu ili kuhakikisha ajira zote zinazotolewa zinazingatia sifa na vigezo vya kuajiri.

Akizungumza katika uzinduzi wa Bodi hiyo mpya jijini Dar es salaam pamoja na mambo mengine, Profesa Mbarawa ameisisitiza bodi hiyo kuifanyia kazi Ripoti ya Uchunguzi wa uendeshaji wa Viwanja hivyo nchini na kufanya mabadiliko mara moja.

“Nataka muipitie ripoti niliyomkabidhi Kaimu Mkurugenzi Mkuu na mufanyie maamuzi, suala la kuajiri watu kiholela, ninataka wote waliandikwa kwenye ripoti hiyo kuwa hawana sifa watolewe wapishwe watu wenye sifa ili waweze kufanya kazi”, amesema Waziri Mbarawa.

Aidha, Profesa Mbarawa ameitaka Bodi hiyo kusimamia kwa uadilifu miundombinu yote ya viwanja vya ndege nchini na kuhakikisha mashine za ukaguzi zinafanya kazi masaa 24 ili kudhibiti mianya yote ya rushwa.Ameitaka Bodi hiyo kusimamia vizuri ukusanyaji wa mapato katika viwanja vyote ili kuweza kufikia lengo lililowekwa na kukuza uchumi wa nchi.

Aidha, Profesa Mbarawa ameitaka Bodi hiyo kushirikiana na wafanyakazi wa Viwanja hivyo katika mambo mbalimbali ili kuboresha utendaji na kuweka uwazi katika utoaji wa huduma katika viwanja hivyo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Profesa Ninatubu Lema amemhakikishia Waziri huyo kuwa ataongeza ushirikiano na wafanyakazi wote na kusimamia maagizo yote yaliyotolewa.Ameahidi kuboresha huduma katika viwanja vyote nchini na kusema kuwa umuhimu wake utaongeza mapato katika viwanja hivyo na nchi kwa ujumla.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa akisisitiza jambo wakati wa uzinduzi wa Bodi mpya ya Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA). Kulia ni Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Prof. Ninatubu Lema.
Wajumbe wa Bodi wakimsikiliza Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa(hayupo pichani), wakati wa uzinduzi wa bodi hiyo jijini Dar es salaam.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa (kushoto) akimkabidhi vitendea kazi Mwenyekiti wa Bodi hiyo ya Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TAA) Prof. Ninatubu Lema (kulia) wakati wa uzinduzi wa Bodi mpya.
Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TAA) Prof. Ninatubu Lema, akifafanua jambo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa (kushoto), wakati wa uzinduzi wa bodi hiyo. Kulia kwake ni MKurugenzi wa Miundombinu ya Uchukuzi, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Eng. Hussein Mativila.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...