Na Chalila Kibuda, Globu ya jamii

Waziri wa elimu, sayansi Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako amesema wananchi wa Mkuranga wamejitoa katika kupata Mandeleo.

  Profesa Ndalichako wakati kufunga kambi ya kufyatua tofali 45000 kwa ajili ujenzi wa mabweni matano na nyumba tano za walimu katika shule ya sekondari Nassibugani iliyopo kata ya msonga wilaya Mkuranga.

Amesema kuwa wananchi wamejitoa kuhakikisha watoto wanapata elimu bora inayoendana na mazingira. Amesema kuwa nia yake nikuona mkuranga kunapatikana mapinduzi ya Elimu.

Amesema vijana 53 wameamua kumuunga mkono kutokana na kuona njia inaonekana ya kujitoa na kwao katika kusaidia maendeleo ya Taifa.

Amesema ujenzi wa mabweni hayo itakuwa suluhu kwa wasichana  kufanya vizuri.Amesena jitihada zinaendelea kutatua baadhi ya changamoto za Elimu kwa kushirikiana na wananchi.Katika ufungaji wa kambi hiyo Mbunge wa Mkuranga ,Abdallah Ulega amesema nia yake ni kuona maendeleo yanapatikana yenye tija.

Waliohudhuria ufungaji ni Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Evarist Ndikilo, Mkuu wa Wilaya, Filberto Sanga na viongozi mbalimbali.
 


Waziri wa Elimu, sayansi Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako  sambamba na viongozi wengie wa wilaya ya Mkuranfa wakishiriki kufyatulia tofali,wakati wa hafla fupi ya kufunga kambi ya kufyatua tofali 45000 kwa ajili ujenzi wa mabweni matano na nyumba tano za walimu katika shule ya sekondari Nassibugani iliyopo kata ya msonga wilaya Mkuranga. 

 Pichani kushoto ni Waziri wa Elimu, sayansi Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako  pamoja na Mbunge wa Mkuranga Abdallah Ulega wakishriki kwa pamoja kuchanganya mchanga wa kufyatulia tofali,wakati wa hafla fupi ya kufunga kambi ya kufyatua tofali 45000 kwa ajili ujenzi wa mabweni matano na nyumba tano za walimu katika shule ya sekondari Nassibugani iliyopo kata ya msonga wilaya Mkuranga. 

 Waziri wa elimu, sayansi Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako akizungumza na wananchi wa Mkuranga wakati wa kufunga kambi ya kufyatua tofali 45000 kwa ajili ujenzi wa mabweni matano na nyumba tano za walimu katika shule ya sekondari Nassibugani iliyopo kata ya msonga wilaya Mkuranga.

Mbunge wa jimbo la Mkuranga, Abdallah Ulega 
akizungumza na wananchi wake wakati wa kufunga kambi ya kufyatua tofali 45000 kwa ajili ujenzi wa mabweni matano na nyumba tano za walimu katika shule ya sekondari Nassibugani iliyopo kata ya msonga wilaya Mkuranga.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...