Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein (kulia)akipokea mmoja wa
Miongoni mwa Misahafu elfu kumi iliyotolewa na Mfalme wa Morocco,
Mohammed VI,mara baada ya Swala ya Ijumaa iliyoswaliwa leo katika
Msikiti wa Mwembeshauri Mjini Unguja,Mfalme Mohammed VI akiwa katika
ziara ya kibinafsi na ujumbe wake, ambapo amefikia katika Park Hyatt
Hotel- Shangani Mjimkongwe wa Zanzibar,[Picha na Ikulu.]28/10/2016.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein na Mfalme wa Morocco,
Mohammed VI, (katikati) pamoja na Viongozi mbali mbali na Ujumbe wa
Mfalme wakijumuika na Waislamu wengine wakiswali swala ya Ijumaa
iliyoswalishwa na Sheikh Fadhil Soraga katika Msikiti wa Mwembeshauri
Mjini Unguja,Mfalme Mohammed VI yupo Nchini kwa ziara ya kibinafsi,
[Picha na Ikulu.] 28/10/2016.
Mfalme wa Morocco, Mohammed
VI(kulia) akisalimiana na Katibu wa Mufti wa Zanzibar Sheikh Fadhil
Soraga mara baada ya kuswalisha Swala ya Ijumaa katika Msikiti wa
Mwembeshauri Mjini Unguja,Mfalme Mohammed VI yupo Nchini kwa ziara ya
kibinafsi, [Picha na Ikulu.] 28/10/2016.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto) akifuatana na
Mfalme wa Morocco, Mohammed VI, pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Mjini
Magharibi Mhe,Ayoub Mohamed Mahmoud (kulia) wakitoka nje ya Msikiti wa
Mwembeshauri Mjini Unguja baada ya swala ya Ijumaa leo,[Picha na Ikulu.]
28/10/2016.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto) akiagana na
Mfalme wa Morocco, Mohammed VI, mara baada ya kumalizika kwa swala ya
Ijumaa leo katika Msikiti wa Mwembeshauri Mjini Unguja,Mfalme wa
Morocco, Mohammed VI yupo nchini na ujumbe wake kwa ziara ya
kibinafsi,[Picha na Ikulu.] 28/10/2016.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...