Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ndg Abdulrahman Kinana ameitumia salamu za rambirambi familia ya Mwenyekiti Mstaafu wa CCM Mkoa wa Iringa Mzee Tasili Mung’wenya Mgoda aliyefariki dunia jana tarehe 14 Oktoba, 2016 katika Hospitali ya Wilaya ya Mafinga.

Mzee Mgoda amewahi kushika nafasi mbalimbali za uongozi ndani ya TANU baadae CCM na Serikalini ambapo amekuwa Mwenyekiti wa Wilaya ya Mafinga, Katibu wa CCM ngazi ya Wilaya na Mkuu wa Wilaya Mstaafu.

Katika Salamu hizo Ndg Kinana amesema amepokea kwa majonzi na masikitiko makubwa kifo cha Mzee Tasili Mgoda ambaye alikuwa ni sehemu ya hazina ya wazee wa CCM na kwamba anaungana na familia ya marehemu, ndugu na jamaa katika kipindi hiki kigumu cha huzuni ya kuondokewa na mpendwa wao.

WanaCCM tunamuomba Mwenyezi Mungu aiweke peponi roho ya Marehemu Mzee Tasili Mung’wenya Mgoda.  Amina

Imetolewa na:-

SELEMAN Y. MWENDA
Kny: MSEMAJI WA CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM)
15/10/2016

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...