Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Samsung Afrika Mshariki,
Nandakishore Nair (kulia) akipiga makofi mara baada ya Rais wa
Chama cha Wabunifu Majengo, Henry Mwoleka kukata utepe
wakati wa uzinduzi rasmi wa bidhaa hizo uliofanyika katika
Hoteli ya Hyatt Kilimanjaro Dar es Salaam jana.
Rais wa Chama cha Wabunifu Majengo, Henry Mwoleka na
(kushoto) na Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Samsung Afrika
Mshariki, Nandakishore Nair wa pili (kushoto) wakipata
maelezo kutoka kwa Afisa masoko wa Kampuni ya Samsung,
Mhandisi, Meshack Odhiambo mara baada ya uzinduzi wa AC
mpya za Kampuni ya Samsung iliyofanyika katika Hotel ya
Hayatt Kilimanjaro Dar es Salaam jana.
Kampuni ya Kielektronikia ya Samsung Afrika
Mashariki, imezindua kiyoyozi chake kipya chenye vifaa vya 360 Cassette, DVM Chiller,
next generation DVM S 30 HP, pamoja na kifaa cha pembeni cha kutolea maji/hewa
(VRF unit) – the DVM S Eco 14 HP.
Kwa pamoja, huu ubunifu wa hivi vifaa vipya (360 Cassette, DVM Chiller, next generation DVM S
30 HP, pamoja na kifaa cha pembeni cha kutolea maji/hewa (VRF unit) – the DVM S Eco 14 HP)
utabadili hali ya sasa ya viyoyozi hususani kwenye ongezeko la nishati, ufanisi na
utendaji, uchukuaji mdogo wa nafasi pamoja na kuongeza kasi ya upatikanaji wa
ubaridi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...