Na Humphrey Shao, Blog ya Jamii

SERIKALI imesema itaendelea kuisadia ofisi ya Mkemia mkuu kuwa na Vifaa vya kisasa ili iweze kupambana na changamoto mbalimbali za upimaji.

Hayo yamesemwa jioni ya leo na Naibu Waziri wa Afya ,Dk Hamisi Kigwangwala katika hotuba yake iliyosomwa na afisa utawala wa Wizara hiyo,Michael John katika hafla ya kukabidhi vyeti kwa wanafunzi waliofanya vizuri katika masomo ya Sayansi Kidato cha nne na cha Sita Mwaka jana.

“Tunashukuru kwa kazi mnayofanya na sisi kama serikali tunajipanga kwa kila namna kuhakikisha kuwa ofisi hii ya mkemkia mkuu inakuwa bora zaidi licha kutangazwa kuwa ndio bora kwa Afrika Mashariki” amesema

Alimaliza kwa kuwataka wanafunzi wote waliofanya vizuri katika masomo yao kuwa bado wanakazi kubwa ya kuongeza juhudi hili kufikia malengo waliyojipangia.

Afisa Utawala wa Wizara wa Afya, Michael John akikabidhi cheti kwa mshindi wa kwanza wa masomo ya Sayansi kwa Wanaume Mugisha Lukambuzi kutoka shule ya Sekondari ya Bendel Memorial ya Moshi
Afisa Utawala wa Wizara wa Afya, Michael John akikabidhi cheti kwa mshindi wa kwanza wa masomo ya Sayansi kwa Wanawake Naomi Sarakikya kutoka shule ya S't Mary's Mazinde juu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...