Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Eng. Ramo Makani (kulia) akizungumza na waandishi wa habari (hawako pichani) hivi karibuni Makao Makuu wa Wizara hiyo Mpingo House juu ya ufafanuzi wa kuwaondoa wananchi katika maeneo yaliyohifadhiwa. Kulia kwake ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Mhandisi Angelina Madete na Mkurugenzi wa Mipango na Matumizi Endelevu ya Rasilimali za Misitu wa TFS, Mohammed Kilongo.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Eng. Ramo Makani (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari (hawako pichani) Makao Makuu wa Wizara hiyo Mpingo House hivi karibuni juu ya ufafanuzi wa kuwaondoa wananchi katika maeneo yaliyohifadhiwa. Kulia ni Mkurugenzi wa Idara Wanyamapori, Prof. Alexander Songorwa.
_____________________________
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Wizara ya Maliasili na Utalii
TAARIFA KWA UMMA
UFAFANUZI
KUHUSU UONDOAJI WANANCHI KATIKA MAENEO YALIYOHIFADHIWA
Serikali
inawakumbusha wananchi wote na kusisitiza kwamba ni wajibu wao kutii sheria na
kuepuka kabisa vitendo viovu vinavyosababisha kupotea kwa uoto wa asili kwa
kasi inayoendelea hivi sasa nchini na kutishia UHIFADHI ENDELEVU, hali hii inapelekea nchi kuwa Jangwa kutokana
na ukataji wa miti hovyo, kilimo kisichoendelevu, uchungaji holela wa mifugo, uanzishaji
makazi na shughuli zingine za kibinadamu katika maeneo yaliyohifadhiwa ikiwa ni
pamoja na Hifadhi za Misitu, Mapori ya Akiba, Mapori Tengefu na Hifadhi za Taifa.
Ikumbukwe kwamba
takwimu zinaonyesha kuwa kwa sasa Tanzania inapoteza takriban hekta 372,000 za
uoto wa asili kila mwaka na kwamba kasi hiyo ikiachwa iendelee tishio la
kutoweka kwa uoto huo ni kubwa sana. Takwimu pia zinaonyesha kuwa Tanzania ina
eneo la uoto wa asili lenye ukubwa wa takriban Hekta milioni 48.1 na kwamba
kasi iliyopo ya uharibifu ikiachwa iendelee itaiacha Tanzania bila uoto wa
asili baada ya miaka 129.
Takwimu hizi
zitabakia hivyo ikiwa idadi ya watu haitaongezeka, ukuaji wa shughuli za
kibinadamu hautaongezeka na aina ya shughuli hizo haitabadilika, jambo ambalo
haliwezekani. Hivyo basi upo uwezekano wa idadi ya miaka hiyo kupungua hata
kufikia nusu, sawa na umri wa kawaida kabisa wa binadamu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...