Sheikh  Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Sheikh Alhadi Mussa Salim (wa tatu kutoka kushoto) akiongoza matembezi ya Amani ya kuadhimisha kifo cha Mjukuu wa Mtume Muhammad (s.a.w.w) ambae ni Imam Hussen (a.s) leo jijini Dar es Salaam. Siku ya mwezi 10 Muharram inajulikana kama ni siku ya Ashura. Imamu Husain (a.s.) aliuliwa kikatili pamoja na wafuasi wake wachache na ndugu zake. Masaibu haya yalitokea zaidi ya miaka 1300 iliyopita huko Kerbala (karibu na mji wa Baghdad katika nchi iitwayo Iraq hivi sasa). 
 Sehemu ya maelfu ya Waumini wa dini ya kiislamu wakiwa katika matembezi ya Amani ya kuadhimisha kifo cha Mjukuu wa Mtume Muhammad (s.a.w.w)  Imam Hussen(a.s) leo jijini Dar es Salaam.
 Matembezi yakiendelea leo jijini Dar es Salaam.
 Mzungumzaji na Kiongozi Mkuu wa Waislam Shia Ithnasheriya Tanzania,Sheikh Hemed Jalala akizungumza na waandishi wa habari wakati wa  matembezi ya Amani ya kuadhimisha kifo cha Mjukuu wa Mtume Muhammad (s.a.w.w) Imam Hussen(a.s) leo jijini Dar es Salaam.
Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Sheikh Alhadi Mussa Salim akizungumza wakati wa  matembezi ya Amani ya kuadhimisha kifo cha Mjukuu wa Mtume Muhammad (s.a.w.w) Imam Hussen(a.s) leo jijini Dar es Salaam. Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...